MCHUNGAJI THOMAS DIGE AWA ASKOFU WA JIMBO LA DAR ES SALAAM. P A G.

Askofu Mpya wa jimbo la Dar es salaam Thomas Dige akizungumza wakati ya hafla ya kumsimika rasmi akichukua nafasi ya Askofu Elly Mwende aliyestaafuJimbo hilo la Dar es salaam linajumuisha mikoa 9 ya Serikali  ambayo ni Dar es salaam, Lindi, Pwani, Mtwara pamoja na mikoa Miwili ya Pemba  na mikoa mitatu ya Unguja.
Mchungaji Thomas Dige wa kanisa la Pentecostal Assemblies of GOD , Mbezi beach amesimikwa rasmi kuwa askofu wa jimbo la Dar es salaam na Zanzibar wa kanisa la Pentecostal Assemblies of GOD( P A G). Nafasi ameipata baada ya uchaguzi mkuu wa kanisa hilo ambapo anachukuwa nafsi ya Askofu Elly Mwende ambaye amestaafu. Askofu Mwende amekuwa askofu wa jimbo hilo kwa muda wa miaka 12 yaani toka mwaka 2001 hadi mwaka huu wa 2013, amefanya mengi sana katika jimbo hilo kwani kipindi anaingia madarakani alikuta makanisa 4 tu yakiongozwa na kanisa mama la DPC yaani Dar es salaam Pentecostal Church, lakini hadi anastaafu leo ameacha makanisa 29 katika jimbo hilo.Askofu Dige ambaye amechaguliwa kuwa askofu kabla ya cheo hicho kipya alikuwa ni katibu wa jimbo wa  kanisa hilo. Pia amechaguliwa askofu msaidizi ambaye ni mchungaji Noel Tabejo kutoka Mkoa wa Pwani na katibu mkuu wa jimbo Mchungaji Gradius Theonest wa Tegeta PAG . licha ya viongozi hao wamechaguliwa pia waangalizi wa kanda ambapo Mchungaji Amos Lukanula amekuwa mwangalizi upande wa Unguja na Pemba pamoja na wengine katika kanda zingine za Lindi na Mtwara. na wajumbe ni pamoja na Mchungaji Elly Boto wa Kawe Pentecostal Church (KPC) . Kiongozi mkuu kutoka ngazi ya Taifa  na msimamizi alikuwa ni Katibu mkuu wa PAG Tanzania na ambaye pia ni Mkuu wa chuo za Biblia cha Mwanza, ndugu Primus Ngeiyamu.zifuatazo picha za tukio hilo la kumpata askofu mpya pamoja na wasaidizi wake.

Katibu mkuu  wa kanisa la PAG na mkuu wa chuo cha Biblia Mwanza Mchungaji Primus Ngeiyamu ambaye ndiye alikuwa msimamizi wa tukio hilo  akiwapa nasaha viongozi wapya wa jimbo la Dar es salaam na katikati ni askofu aliyestaafu, Elly Mwende

Baadhi ya wachungaji na maaskofu wakisikiliza neno la MUNGU kutoka kwa Mchungaji Primus Ngeiyamu

Kutoka kushoto, askofu msaidizi Noel Tabejo, Askofu Thomas Dige na askofu aliyestaafu Elly Mwende

Askofu mstaafu Elly Mwende akizungumza machache ikiwemo mafanikio rukuki wakati wa uongozi wake kabla ya kukabidhi rasmi madaraka kwa askofu Thomas Dige





Wachungaji, wakuu wa idara wapya wa kanisa la PAG jimbo la Dar es salaam wakiombewa na kuwekwa wakfu kwa kazi ya MUNGU

Kutoka kushoto, Askofu mpya wa jimbo la Dar es salaam Thomas Dige, katikati ni Mchungaji Paul Safari na kulia ni Askofu aliyestaafu Elly Mwende wakati maombi yakiendelea. Jimbo hilo la Dar es salaam linajumuisha mikoa 9 ya Serikali  ambayo ni Dar es salaam, Lindi, Pwani, Mtwara pamoja na mikoa Miwili ya Pemba  na mikoa mitatu ya Unguja.



Askofu Thomas Dige baada ya kuwa askofu mpya wa jimbo la Dar es salaam

Askofu anayestaafu Elly Mwende akimkaribisha rasmi askofu mpya Thomas Dige







Askofu mpya Thomas Dige, askofu aliyestaafu Elly Mwende na Mkuu wa chuo cha Biblia Mwanza Primus Ngeiyamu wakimuombea Mchungaji Amos Lukanula ambaye ndiye mwangalizi wa kanisa hiyo kule Unguja na Pemba. kanisa lake liko Chukwani , Zanzibar

Askofu msaidizi Noel Tabejo akiombewa.

Mkurugenzi mpya wa vijana wa jimbo akiombewa

Mkurugenzi mpya wa Wamama wa jimbo akiombewa





ilikuwa ni shangwe , hapa ni Pastor Mpapai akiimba

Askofu  Thomas Dige akimwombea Mchungaji Paul Safari ambaye ni mjumbe


Baada ya hayo yote ilikuwa ni kula na kula na kushiba katika jina la YESU

Comments