MOROGORO KUTIKISWA NA YESU KRISTO KUPITIA UFUFUO NA UZIMA


Mchungaji Josephat Gwajima, Ufufuo na uzima
Baada ya mikutano iliyovunja rekodi kwa idadi ya watu yaani Arusha, Moshi na Tanga; sasa kanisa la Ufufuo na Uzima linahamishia mikutano yake mkoani Morogoro ambapo Mchungaji Gwajima ambaye pia ni mchungaji kiongozi wa kanisa hilo anatarajiwa kuhubiri kwa siku nane mfululizo. 

Pamoja Mchungaji Gwajima atafuatana na timu ya watendakazi zaidi ya mia tatu na waimbaji maarufu wa injili kama Flora Mbasha, John Lisu, Jackson Benty na Mwanamapinduzi Band. 

Mkutano huo wa kwanza kufanyika Morogoro kwa kanisa la Ufufuo na Uzima unatarajiwa kushuhudia misukule wakirudi, wagonjwa wakipona, viwete wakitembea na mambo mengine mengi ya ajabu. 

Hapa ilikuwa ni mkutano wa Tanga siku chache zilizopita
huu ni mmoja wa miujiza ambayo BWANA YESU aliitenda Arusha kupitia ufufuo na uzima
Usikose kuhudhuria na wewe ili kupokea muujiza wako.


Comments