PAPA ASHEREHEKEA BIRTHDAY YAKE NA WASIOJIWEZA

Papa Francis ©catholicvirtue

Papa Francis wa kanisa Katoliki duniani amesherehekea siku yake ya kuzaliwa kwakuwakaribisha watu wasiojiweza wanne ambao walijumuika na wageni wengine pamoja na Papa kupata kifungua kinywa alichoandaa mahususi kwa kutimiza miaka 77 tangu azaliwe, katika makazi ya Mtakatifu Martha yaliyopo Vatican nchini Italia.

Papa Francis aliwaalika watu hao pamoja na wafanyakazi wa Vatican waliojumuika na familia zao katika makazi hayo ambayo amekuwa akiishi tangu achaguliwe kuwa Papa ambayo pia yamekuwa yakikaliwa na mitume na viongozi mbalimbali wa kanisa hilo. Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na radio ya Vatican imeendelea kuripoti kwamba watu hao ni kati ya kundi kubwa la watu wasio na makazi ambao hulala nje ya viunga vya Mtakatifu Peter.

Aidha katika picha zilizotolewa zimemuonyesha Papa Francis akizungumza na watu watatu kati ya wanne aliowaalika akiwemo mmoja aliyeonekana akiwa amembeba mbwa. Taarifa ya Vatican imesema tukio hilo lilikuwa lakirafiki zaidi huku waziri wa mambo ya ndani wa Vatican Pietro Parolin amemtakia heri Papa Francis katika siku yake ya kuzaliwa.

Papa akiwa na watu wasio na makazi nje ya Vatican ©cbcnews
chanzo:gospel kitaa

Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments