TAMASHA KUBWA LA KUANZA MWAKA NA BWANA PTA SABASABA

Kwa habari zilizoenea mjini, ni kwamba kila mtu jijini anapanga kufika kwenye ibada ya kuanza mwaka na Bwana kwenye kanisa la EAGT City Centre chini ya Mchungaji Florian Katunzi, ambapo kutakuwa na tamasha kubwa sana la changizo kwa ajili ya ujenzi wa kanisa kubwa zaidi ya ukumbi wa Sabasaba ambao unatumika kwa hivi sasa.

Waimbaji nio wengi, na ni sahihi kusema karibia waimbaji wote Dar watakuwepo siku hiyo, kuanzia walichapwa kwenye karatasi za matangazo hadi wale ambao hawajaainishwa, ikiwemo Upendo Nkone, Masanja Mkandamizaji, Beatrice Mwaipaja, Christina Mbilinyi, Anne Annie, na wengineo wengi. Yote haya ni kuanzia saa nane mchana na kuendelea kwa kiingilio cha 5,000 kwa watoto, 10,000, 20,000 na 50,000.

Karibu uchangie huduma ya Neno la Mungu isonge mbele, na pia upate huduma ya maombezi kutoka kwa mtumishi wa Mungu, Florian Katunzi, by Power, by Force.
Chanzo:Gospel kitaa
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12