Cecilia Ricardo, binti aliyepofuka macho akiwa mdogo, aliyetamani kujiua 
            
Ilikuwa mwaka 2011 mwezi wa saba katika eneo la 
Visole Manispaa ya Morogoro, Cecilia Ricardo anasema kuwa wakati huo 
akiishi kwa dada yake, Theresia Patrick Ricardo alimtuma mtoto wa dada 
yake, Evodia kwenda dukani kununua sumu ya kuua panya ili anywe kwa 
lengo la kujiua, maamuzi hayo alichukua kutokana na mateso yaliyotokana 
na maumivu makali ya macho ambayo baadaye yaliyopoteza kabisa uwezo wa 
kuona hadi leo.
                
              
Zilikuwa siku nne za mateso makali ya maumivu 
ikiambatana na maumivu ya kichwa mfulululizo na macho kutoka maji, hali 
ambayo ilimshawishi kumtuma mtoto aende dukani kununua sumu ya panya ili
 kujiua.
                
              
Hata hivyo mtoto huyo alifichua siri hiyo kwa kaka
 aliyekuwa nje na kunyang’wa fedha na kwa sababu hakuwa na uwezo wa 
kuona mbinu yake ya kuijua iliishia hapo, anasema Cecilia katika 
mahojiano na mwandishi wa makala haya eneo la Madizini Kilakala mkoani 
Morogoro.
                
              
Cecilia anaeleza namna mkasa huo ulivyomtokea 
baada ya kutoka katika mji mdogo wa Turiani Wilaya ya Mvomero mwezi 
mmoja baada ya kufika kwa dada yake Manispaa ya Morogoro kwa lengo la 
kujipumzisha huku akiwa amebeba kiasi cha fedha Sh30,000 fedha alizopata
 kutokana na mradi wa kuuza maji baridi.
                
              
Baada ya kuishi Morogoro Mjini kwa muda wa mwezi 
mmoja aliona upo umuhimu wa kuwasiliana na familia iliyoko Turiani hivyo
 njia pekee ya kuwasiliana nao ni kununua simu ya kiganjani ndipo 
alipomwambia dada yake kumpeleka mjini ili akanunue yenye uwezo wa 
kuweka nyimbo ili kuweza kupata nafasi ya kuweka nyimbo za injili.
                
              
“Nilinunua simu dukani na kwenda kusajiliwa lakini
 nilimwomba dada niwekewe nyimbo za injili ikiwa njia moja wapo ya mimi 
kuniriwaza pindi ninapokuwa na mawazo juu ya maisha yangu hasa baada ya 
kupoteza kabisa uwezo wa kuona,” anasema Cecilia huku akiwa mwenye 
furaha na kuonyesha tabasamu.
                
              
Anasema kuwa wakati wamefika eneo la kibanda cha 
kuweka nyimbo katika simu yake, Cecilia alichagua nyimbo nyingi za kwaya
 ya Kanisa la Katoliki, jambo hilo lilimpa mshangao mmiliki wa kibanda 
hicho, Noah Mgeni na kuhoji kwa nini dada huyo amekuwa akitoa masharti 
ya kutoingiza nyimbo nyingine tofauti na nyimbo za injili tu.
                
              
Theresia Patrick Ricardo dada mkubwa wa Cecilia 
alimwondolea mshangao huo Noah kwa kumweleza kuwa huyo mdogo wake ni 
mlemavu wa macho (haoni kabisa) na hapo kabla ya kupata ulemavu huo 
alikuwa mwanakwaya hivyo njia pekee ya kujiliwaza kutokana na ulemavu 
huo ni kusikiliza nyimbo za kwaya.
                
              
Noah aliendelea kuhoji je, anaweza kuimba na 
kucheza licha ya kuwa mlemavu... Kama anaweza basi mimi nitamuunganisha 
na mtu ili aweze kutumbuiza katika kumbi za sherehe za harusi, kipaimara
 na kadhalika.
                
              
“Baada ya kugundua Cecilia kuwa ni mlemavu wa 
macho, nilimwomba namba yake ya simu ili nimuunganishe na yule mtu 
ambaye niliamini angeweza kumsaidia,” anasema.
                
              
Noah anaeleza kuwa baada ya kupata namba ya simu 
ya Cecilia alimpigia na kufunga safari ya kumtembelea nyumbani kwa dada 
yake Visole ambako alikuwa anaishi
                
              
kwa lengo la kumfahamu zaidi na hilo alilifanya na
 kumvutiwa naye huyo dada kwa sababu yeye ni msanii na alikuwa anaigiza 
kucheza muziki wa injili kama mlemavu wa macho.
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12
“Baada ya kuonana naye Cecilia kwa mara ya pili nyumbani kwao, 
nilimshauri kuwa kutokana na umbo alilokuwa nalo, ni vizuri zaidi kama 
atakuwa anacheza, naye akakubali,” anasema.
Noah alisema kuwa alianza kumfundisha kucheza, 
wimbo wa kwanza ni ule wa wasanii wa muziki wa injili kutoka nchini 
Burundi wa kwaya ya Ambasado kupitia wimbo wa kwetu pazuri na aliweza 
kumudu vema kucheza kwa hisia jambo ambalo yeye Noah alikuwa analitaka.
“Mimi ni msanii na ninacheza katika sherehe 
mbalimbali zikiwemo harusi, nacheza nyimbo za injili tu na kuigiza kama 
mtu nisiyeona na wageni waalikwa hunitunza fedha, lakini nilipogundua 
Cecilia ni mlemavu wa macho niliona bora nafasi hiyo awe anacheza yeye 
kwa uhalisia tofauti na mimi hicho ndicho chanzo cha binti huyu kuingia 
fani ya kucheza muziki”anafafanua Noah.
Cecilia Joseph Ricardo anasema mawazo ya kutaka 
kujitoa uhai kwa kunywa sumu ya panya kwa sasa hayapo tena katika kichwa
 chake, ni kutokana na ushawishi wa Noah Mgeni ambaye amembadilisha kwa 
kumwingiza katika fani ya muziki.
“Sasa hivi nimepata faraja kubwa kupitia muziki wa
 nyimbo na nimekuwa nikicheza show katika sherehe za harusi na wasamalia
 wema wamekuwa wakinitunza fedha ambazo natumia katika kuendesha maisha 
yangu mwenyewe bila utegemezi wowote kutoka kwa wazazi wangu akiwemo na 
dada yangu na nina amani sana moyoni na huu upofu ni kama makusudi yake 
katika mitihani kama binadamu wengine” anasema Cecilia.
Kuna aina nyingi za ulemavu na kukumbwa na 
changamoto mbalimbali katika jamii inayoizunguka lakini wapo ambao 
wanaweza kufanya jambo la kuweza kuendesha maisha yao wenyewe bila 
kuhitaji utegemezi labda kuwezeshwa nyenzo tu na mambo mengine kufanya 
wenyewe hilo linawezekana endapo kutakuwa na mtu wa kukushika mkono,” 
anafafanua.
Hali ilivyokuwa awali 
Cecilia anasema kuwa yeye kabla ya macho yake 
kupoteza kabisa nuru ya kuona alikuwa na malengo mengi kama binadamu 
wengi na kati ya malengo hayo ni kuwa mtawa; enzi za utoto wake alikuwa 
mwimbaji katika kwaya ngazi ya shule na kanisa Katoliki.
Amekuwa akipenda wasanii wakubwa wa nyimbo za 
injili wakiwemo Christina Shusho hasa kupitia wimbo wake wa Nipe Macho, 
Anastazia Mkobwa katika wimbo wa Nishike mkono na Ambasada wimbo wa 
kwetu pazuri.
Alivyopata ulemavu 
Akiwa na umri wa miaka 10 akisoma darasa la tatu 
shule ya msingi Mtibwa wakicheza mchezo wa kujaza mchanga kwenye chupa 
ya soda na wenzake saa 7 mchana siku ya jumamosi eneo la kanisa la 
Anglikana, mtoto Ambe Oden alirusha mpira wakati yeye Cecilia Ricardo 
akijaza mchanga huku amekaa chini katika chupa, alikwepa mpira huo na 
uso wake kugonga katika mdomo wa chupa katika jicho lake la kushoto.
Cecilia anasema kuwa baada ya kuinamisha uso wake 
wakati akikwepa mpira uliorushwa na Ambe Oden na kujibamiza katika jicho
 la kushoto, aliona nyota nyingi usoni katika macho yote na maumivu 
makali na mchezo uliishia hapo. Baadaye wenzake walimshika mkono na 
kumrudisha nyumbani huku macho yakipoteza nuru ya kuona, na maumivu 
makali.
Baada ya dakika 10 baadaye macho yake yalirejea katika hali yake
 ya kawaida na kuanza kuona huku yakiwasha na maumivu yalidumu kwa siku 
mbili na macho yakiwa yamevimba, anafafanua.
Siku ya tatu tangu apate tatizo hilo alipelekwa 
hospitali ya misheni ya Bwagala Turiani, hiyo ilikuwa mwaka 2000, 
alipimwa na kugundulika kuwa ana presha ya macho na kutakiwa kufanyiwa 
operesheni.
Alilazwa kwa siku mbili na siku ya tatu hatimaye 
alifanyiwa operesheni katika jicho la kulia badala ya kushoto na siku ya
 saba baada ya kufanyiwa operesheni alirejea nyumbani na kuendelea na 
masomo ya shule ya msingi huku macho yakiwa katika nuru mzuri ya kuona, 
ikiwa ni baada ya kufanyiwa oparesheni lile lililoumia.
Anawataja watoto wenzake enzi hizo kwa kutaja timu
 ya mchezo huo wa kujaza mchanga katika chupa baina ya mtaa wa kanisani 
na bondeni kwa majina, katika timu yake ya kanisani iliwakilishwa na 
yeye, Jamhuri Seif, Mwajabu Sufian, Ramadhan Wania, Ruth Elias, 
Christina Daniel na Christina Anthony.
Wakati timu ya wapinzani wao iliundwa na Amba 
Oden, Patrick Richard, Mariam Seif, Winfrida Anthony, Halima Abdallah, 
Anna Anthony, Mwanahamis Sufian, Jesca Pius na Georgina Kulabuku ambao 
wamefariki dunia.
Hali inajirudia 
Akiwa darasa la tatu mwaka 2006 macho yake 
yalianza kupoteza tena uwezo wa kuona taratibu. Alilazimika kuomba 
kuomba ahamishiwe kutoka dawati la nyumba ambako alikuwa anakaa na 
kuhamia mbele ili kuweza kuona kilichoandika ubaoni.
Kabla ya likizo ya mwezi wa sita akiwa kidato cha 
pili shule ya sekondari ya kata ya Turiani wilaya ya Mvomero mkoani 
Morogoro akiwa na umri wa miaka 16, licha kusogezwa dawati la mbele ili 
kuweza kuona kilichoandikwa ubaoni wakati huo ikiwa ni mwezi wa tano 
mwaka 2006 dawati lake tena lilisogezwa jirani na ubao ambako maandishi 
yalikuwa anaona.
Hali imeendelea kuwa mbaya kadri muda ulivyokuwa 
unaenda mbele, hata baada ya kurudishwa hospitali, hakuweza tena kuwa na
 uwezo wa kuona.
Mama mzazi wa Cecilia Patrick Ricardo, Evodia Lucas (53) anasema suala hilo anamuachia Mungu.
Evodia anasema baadhi ya madaktari walisema tatizo
 la mwanaye amerithi kutoka kwa bibi yake lakini jambo hilo yeye 
anapinga akida hakuna mwenye tatizo hilo ukiachilia mbali kwa mama yake 
na mtoto wake tu.
Source: Mwananchi
Source: Mwananchi
Comments