HAKIKISHA JINA LAKO LIMEANDIKWA KWENYE KITABU CHA UZIMA.



Siku hizi watumishi wengi na waumini wanadhani kuwa na karama ndiyo tiketi ya kuwa mtakatifu au kuwaleta kwa Yesu, Paulo alishaonya ya kuwa asije akawahubiri watu wengine lakini yeye akataliwe 1Kor 9:27.Kwa hiyo tusijifu kwa karama alizotupa Mungu bali majina yetu kuwa yameandikwa katika kitabu cha uzima Luka 10:20 pia tusiangaikie vitu vinavyoonekana bali visivyoonekana 2Kor 4:18 vilevile tuutafute ufalme wa Mungu Mathayo 6:33.Kumbuka Mungu wetu ni Mtakatifu kwa anatutaka tuwe watakatifu 1Petro 1:16.Hatujachelewa kwani Mungu anachotaka ni sisi huwa watakatifu na kutakasika tunahitaji toba ya kweli yaani




1.Kujutia dhambi zetu
2.Kumaanisha kuziacha dhambi.
3.Kubadilika kuwa kiumbe kipya.
4.Kuanza mwanzo mpya ili watu wakituona wamtukuze Mungu.
Ndiyo maana atuhakikushia kutofuta majina yetu kwenye kitabu cha uzima Ufunuo 3:5.Tukipenda tusifiwe hapa dniani bila majina yetu kuandikwa siku ya hukumu pamoja nautumishi mzito tutakataliwa Mathayo 7:22,2Kor 9:27




                          By Evangelist Erick Mwasyoge.

 
 Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments