KAMA UNATAKA UZIMA WA MILELE MPE YESU MAISHA YAKO.





BWANA YESU asifiwe, karibu.
Matendo 4:12
‘’Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.’’
Ila ni jina YESU KRISTO.
Ila ni jina la YESU KRISTO.
Ila ni jina la YESU KRISTO.

Walikuwepo mitume wengi ila hawakuweza kuokoa.
Walikuwepo manabii wengi hawakuweza kuokoa.
Walikuwepo watu maarufu ila hawakuweza kuokoa.
Walikuwepo walimu wa dini ila hawakuweza kuokoa.
Ila ni jina la BWANA YESU pekee ambalo tunaweza kuokolewa kwalo.
Biblia inaweka wazi juu ya nani ambaye anaweza kuwafanya wanadamu wasiende jehanamu

Warumi 10:9-13.  ‘’Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika.  Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni BWANA wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao;
 kwa kuwa, KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA.’’
Ndugu  zangu BWANA YESU anaokoa na ukiamini hakika unaokoka maana hakuna uzima kwingine.
Yohana 14:6 Biblia inasema ‘’ YESU akamwambia, Mimi ndimi njia , na ukweli na uzima; mtu haji kwa BABA ila kwa njia ya mimi.
Ndugu yangu mpendwa kuokoka ni lazima kwa kila anayeutaka uzima wa milele.

BWANA YESU leo anasema.
‘’Njooni kwangu nyote, wenye kulemewa wenye kulemewa na mizigo nanyi nitawapumzisha.
Wenye mizigo ya magonjwa, njooni kwangu nami nitawapumzisha.
Wenye mizigo ya madeni njooni kwangu , nami nitawapumzisha.
Wenye mizigo ya kuteswa na wachawi njooni kwangu nami nitawapumzisha.
Wenye kuonewa na mapepo, njooni kwangu , nami nitawapumzisha.
Wanaoteswa na mizimu na roho za ukoo, njooni kwangu nami nitawapumzisha.’’

KWANINI BWANA YESU PEKEE?

Ni BWANA YESU pekee wa kuokoa kwa maana MUNGU alimtoa kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu, ukombozi wa mwili na roho pia.Yohana 3:16-18 ‘’Kwa maana jinsi hii MUNGU aliupenda ulimwengu ,  hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.   Maana MUNGU hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu,  ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye  yeye hahukumiwi, asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina  la mwana pekee wa MUNGU.
BWANA YESU alidhihirishwa ili azivunje kazi za shetani(1 Yohana 3:8b).
Ndio maana ukiwa ndani ya KRISTO umekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya. -2 korintho 5:17.
                               MUNGU akubariki sana.
                                   Ni mimi ndugu yako.
                                       Peter M Mabula
                              Maisha ya ushindi Ministry

 
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments