Ndoto na mapana yake.




BWANA YESU asifiwe watu wa MUNGU.

Ni nafasi mpya MUNGU amenipa ili tujifunze jambo muhimu sana katika maisha ya mwanadamu, jambo hilo ni ‘’NDOTO’’

Karibu.

-Jinsi unavyoonekana katika hali ya mwili inaonyesha ulivyo katika ulimwengu wa roho. Kamwe huwezi kuwa tofauti na jinsi ulivyo katika ulimwengu wa roho.

-Maarifa uliyonayo huanzia katika ulimwengu wa roho na sio katika ulimwengu wa mwili japokua unasoma katika mwili lakini asili yake ni katika ulimwengu wa roho.

-Mambo yakikataliwa katika ulimwengu wa roho lazima yatagoma pia katika ulimwengu wa mwili.

-Hali ya ulimwengu wa roho huongoza ulimwengu wa mwili au ulimwengu huu unaoonekana. Hebu ona, roho yako inapotengana na mwili hutokea kifo na hakuna mwanadamu anayeweza kukurudishia tena uhai wako, labda iwe kwa nguvu za kiroho. Na huo ndio muujiza uupatao kila siku.

DIRECTOR. PETER MICHAEL MABULABiblia imeanisha ndoto 34, kati ya hizo 22 ziko agano la kale na 12 ziko agano jipya.

                 BAADHI YA NDOTO KATIKA AGANO LA KALE.
Abimeleki, kuhusu Sara (Mwanzo 20:3)

Yakobo, kuhusu ngazi (Mwanzo 28:12)

Yakobo, kuhusu Misri (Mwanzo 46:2)

 Labani, kuhusu Yakobo(Mwanzo 31:24)

 Yusufu , kuhusu wazazi wake na ndugu zake (Mwanzo 37:5)

 Yusufu, kuhusu jua, mwezi na nyota (Mwanzo 37:9)

Mnyweshaji mkuu wa mfalme, kuhusu yeye mwenywe(Mwanzo 40:9).

                      BIBLIA IMEANDIKA WAOTA NDOTO 14.

1. Abimeleki (Mwanzo 20:3-6)

2. Yakobo (Mwanzo 28, 31:10-11)

3. Labani (Mwanzo 31:24)

4. Yusufu (Mwanzo 37:5-10)

5. Mlinzi mkuu wa gereza (Mwanzo 40:9-15)

6. Muokaji mkuu wa mikate(Mwanzo 40:10-23)

7. Farao (Mwanzo 41:32)

8. Wamidiani(Waamuzi 7:13-15)

9. Suleimani (1 Wafalme 33:5-15)

10.                  Nebukadreza (Danieli 2 na 4)

11.                  Danieli (Daniel 2 na 7)

12.                  Yusufu (Mathayo 1:20, Mathayo 1:13-22)

13.                  Mamajusi (Mathayo 2:12)

14.                  Mke wa pilato (Mathayo 27:19)

Nawe pia unaweza kuwa mmoja wa waota ndoto wa kizazi chako.

                 UMUHIMU WA NDOTO.

MUNGU hukuletea ndoto ili kukuelewesha msimamo wako katika ulimwengu wa roho.

      NDOTO NI MAWASILIANO BINAFSI KATI YAKO NA MUNGU WAKO

Ndoto ni kitendo kinachotokea wakati umelala, hii yaweza kutokea usiku au mchana, kama utakuwa hujalala siyo rahisi kujua jambo linaloendelea katika ulimwengu wa roho.

Wakati unapokuwa umelala roho yako huwa na mawasiliano na roho nyingine zilizo hai au unawasiliana na MUNGU katika ulimwengu wa roho ambako mambo yote hutokea.

-Mambo yote yaliyoko katika hu ulimwengu wa mwili, yaani yale unayoyaona  asili yake ni katika ulimwengu wa roho. Hakuna jambo lolote linaloweza kutokea katika ulimwengu wa mwili kabla halijatokea katika ulimwengu wa roho.

MUNGU akubariki sana

Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula

Maisha ya ushindi Ministry




 


Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments