![]()  | 
| Mch Dr Philemoni Tibanenason | 
Mch
 Dr Philemoni Tibanenason ni Mwangalizi mkuu wa Kanisa la Pentekoste 
Tanzania(KLPT),na kwa sasa ni mchungaji wa kanisa la KLPT lililoko Mnazi
 mmoja jijini Dar es salaam.Hapa Mch Dr Philemoni Tibanenason anaeleza 
namna alivyotoka Bukoba hadi kufika jijini Dar es salaam.
“Katika
 Miaka ya Sabini Nilikaa Bukoba nikifanya Huduma kwa miaka 
miwili,Bukoba(Kagera) ndio mkoa nilioanzia huduma, katika kipindi hicho 
nilikuwa na miaka 26,na mke wangu alikuwa na miaka 20.Siku moja nikiwa 
nimelala  yalikuja maono yakinitaka niondoke Bukoba niende eneo lingine 
ambalo ni mbali sana na Bukoba yaani Dar es salaam.Nilipoyaona hayo 
niliwaambia watu waliokuwa karibu nami ikiwa ni pamoja na waumini kwamba
 Imenipasa kwenda kule Mungu alikotaka niende”
Sikulijua
 hilo kama lingepokelewa kwa hisia tofauti na waumini niliokuwa nao 
kipindi hicho,hasa ikizingatiwa walikuwa wakinipenda kwa namna ambayo 
sikuwa najua kwa sababu gani.Nilijua huenda wangefurahia  na kunipa 
mkono wa kwa heri , lakini walisema wasingependa kunipoteza kwamba 
niende mbali na wao.Ilinilazimu kuwa na subira kukaa na kumwachia Bwana 
ili yeye kwa uwezo wake afanye mwenyewe, lakini nikizidi kumsihi Mungu 
kwamba mapenzi ya Mungu yatimizwe na si kama nitakavyo mimi bali kama 
atakavyo yeye.
Jambo
 la kushangaza baada ya kupita muda fulani mke wangu alienda kwenye 
maombi  na huko kulikuwa na watumishi wengine. Alipofika huko hakukuwa 
na mtu aliyekuwa akijua maono yangu ambayo Bwana alisema na mimi ya 
kwamba nihame Bukoma na kuelekea Dar es salaam. Na kipindi hicho 
washirika wangu walikuwa hawataki nihame.
![]()  | 
Dar es salaam Ilivyo sasa 
 | 
Baada
 ya Swali hilo mke wangu alikuwa kimya kisha na baada ya kumaliza maombi
 alirudi nyumbani na kunishirikisha.Aliponiambia habari hizo nikasema 
kwa kweli  kwa namna yeyote ile, iwe kwa Miguu,au gari ni lazima nianze 
safari mara moja ya kwenda Dar es salaam.Washirika niliokuwa nao wao 
waliendelea kushikilia  msimamo wao kuwa kuwa hawataki niondoke.Kwa 
mazingira hayo hawakuwa tayari kunipa nauli walikazania niendelee 
kuhubiri eneo hilo.
Nilikaa
 chini na kujiambia ikiwa nitawasikiliza wao nitakuwa simsikilizi Mungu 
aliye hai,niliangalia namna nitavyoweza  kupata pesa za nauli za kunitoa
 Bukoba hadi Dar es salaam, lakini sikuweza kuiona.Hivyo nikashauriana 
na mke wangu kuwa tuuze kitanda  ili tuanze safari mara moja, kwa Neema 
ya Mungu nilifanikiwa kupata shilingi 100,kwa kipindi hicho pesa hiyo 
 ilikuwa ni kubwa kiasi kwamba hadi kufika Dar es salaam ilitughalimu 
kiasi cha shilingi 45/= tu.
Tulipofika
 Dar es salaam na mke wangu tuliwakuta wamishionari tuliofanya nao kazi 
na wakati wanaondoka walituachia waumini 10, nakumbuka kipindi hicho 
hakukuwa na wahubiri wengi kama kipindi hiki.Kipindi hicho Askofu Moses 
Kulola,Masalu,Emmanuel Lazaro sambamba na Titus Mkama ndio waliokuwa 
wakijitoa mhanga kuihubiri injili jijini Dar es salaam.Kipindi hicho 
Jiji la Dar es salaam lilikuwa limefunikwa na Uislamu na wakati Mwingine
 ilikuwa ni hatari kutembea huku ukiwa umeshika Biblia.
Katika
 Miaka hiyo ya Sabini makanisa ya wokovu jijini Dar es salaam yalikuwa 
Temeke na Ilala na tulikuwa tukifaanya kazi ya Mungu kwa Nguvu,Upendo na
 Ushirikiano mkubwa.Tulifanya kazi hiyo kwa muda mrefu ilipofikia Miaka 
ya Themanini ndipo Mikutano ya Injili ilianza.


Comments