ACHA KUTANGA TANGA.


Wapendwa katika Kristo Yesu Shalom!
Nyakati hizi kama maandiko yanavyosema ni za hatari 2Timotheo 3:1.Kweli ni za hatari kwani kasi ya kuwatafuta na kuweka imani kwa wanadamu imesababisha watu kutanga tanga.Wanafikiri Yesu yuko mbali nao bali wako karibu na wanadamu wanaowatukuza na kujenga imani kwao,lakini wanadamu hao wakishindwa wanakata tamaa.Kwa sababu wameweka kwao kuwa watamaliza shida na matatizo yao.Funguka mponyaji na mmaliza shida na matatizo yetu yote tukijenga imani kwake.Yesu yuko karibu sana nasi tukivunjika
mioyo yetu na kupondeka roho zetu.Zaburi 34:18.Mama mmoja aliyekuwa anaumwa aliweka imani yake kwa Bonke hivyo mtumishi alipokuja akawaambia watoto wake wampeleke kwani Bonke atamponya,lakini kinyume hakupokea uponyaji akakasirika na kukata tamaa kuwa kama mtumishi huyo kashindwa kumponya basi hakuna atakaye mponya.Lakini akili za Mungu hazichunguziki na hazina mipaka.Kanisani kwake uliandaliwa mkutano na mhubiri asiyevuma alitumika,watoto wake walikuwa wameokoka wakambebeleza ahudhurie japo aliendelea kubisha lakini walimwambia si Bonke wala huyo wa sasa hakuna awezaye kuponya bali Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai.Mama alibadili mwelekeo wa imani na kujenga imani kwa Yesu alipoombewa tu alipokea uponyaji wake.Tuache kuweka imani kwa wanadamu bali kwa Bwana Yesu tu Yeremia 17:5.Tuache kutanga tanga tukitafuta uponyaji kwani uko kwetu wenyewe tukiweka imani kwa Yesu tutamwona na kupokea uponyaji na kutuondolea shida na matatizo yetu kwani pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu Waebrania 11:6.







 

 Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments