ATAKUOKOA NA MATESO SITA

Wimbo wa Injili mpya uliotungwa na Robert Maziku umepokelewa vyema na wapenzi wa nyimbo hizo hasa ni mpangilio wa ujumbe uliomo ambao sehemu kubwa umetoka kitabu cha Ayubu 5:19 (Yeye atakuokoa na mateso sita: Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.), Ayubu 14:8-9 Inasema Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo, 9. Lakini kwa Harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama mche.


Robert Maziku anawimbo mmoja tu ambao ameimba kama Single artist Ingawa ni mtunzi na mwalimu mzoefu wa kwaya. Kwaya ambazo alishawahi kuzifundisha ni PRS CHOIR ya Dodoma, Kahama Revival ya Wilayani Kahama, Kwaya ya Casfeta Jamhuri Sekondari (Dodoma), Kwaya ya TAFES Hombolo Dodoma, Amani kwaya ya Heaven of Peace Christian Church (Morogoro) na kwa sasa anafundisha kwaya ya Nazareth katika huduma ya Bethel Jijini Dar-es-salaam.

Wimbo wake huo umerekodiwa katika Studio ijulikanayo ALFA ONE LOVE PRODUCTION chini ya Producer kijana Baraka Nathan huku video ikifanywa na BRG ENTERTANMENT chini ya Director Steve Manrizo.

Kwa mwaliko au kutaka kujua chochote kuhusu kazi hii piga 0653340950

 

 Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments