Na Mtu wa Mungu Nabii Samson Mboya, |
Utangulizi:
Yeremia 1:4 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla
hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. Tangu tumboni Mwa mama mzazi ndipo tunapoanzia kujifunza Mambo mbali
mbali,kwa kuhisi hali ya mazingira tunayotarajia kuja kuishi,
Tunapofika ulimwenguni tunaendelea kujifunza
kwakuhisi,kuona,kusikia, kila kitu, kutofautisha ni pale utapopata Neema ya
Mungu kwakuwa tunaishi katika falme mbili, unapokuwa bado tumboni unaishi
katika falme tatu, Mungu,mzazi,shetani japo falme kuu bado inabaki kuwa ya
Mungu
Falme kuu mbili zinazofanya kazi hapa Duniani,
Ø Ufalme wa Mungu- (Nuru)
Ø Ufalme wa Muovu-(Giza)
Ni vizuri ukafahamu hilo
kwanza kabla ya mengineyo Mengi ,Ufalme wa Mungu Unasimamiwa na Mungu Mwenyewe
Katika Utatu Mtakatifu Mungu Baba,Mwana,na Roho Mtakatifu, katika mambo yote
matakatifu,
Ufalme wa Muovu (Shetani)nao
unasimamiwa na Shetani mwenyewe na majeshi yake,Katika mambo maovu yote,
Falme hizi zote zina fanya kazi katika Ulimwengu wa
ki-Roho na kujidhihirisha katika Ulimwengu unaoonekana kwa Macho ya Damu na
nyama, kwa sababu Maalumu, na Hizi falume zinashindana kila wakati,
Waefeso 6:12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama;
bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya
pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
Mema yote au Mabaya yote yanafanyika kupitia Falme hizi nilizozitaja
hapo juu, Mwanadamu asipotumika katika Mema basi atatumika katika
Mabaya,asipomtumikia Mungu atatumikishwa na Shetani, usiposababisha makwazo
utasababishiwa,
Katika maisha tunayoishi Hapa
Duniani kwakuwa tu wapitaji basi na makwazo hayana budi kutokea ila tunajifunza, kama vile ambavyo mtu Mwema
anavyoweza kujifunza ubaya akawa Mtu muovu ndivyo ambavyo mtu mubaya anavyoweza
kujifunza wema na akawa mtu mwema inategemea unajifunza kwa nani, kwa Mungu au kwa Shetani
Mwenye sifa ya kusamehe dhambi Maandiko yameweka wazi ni
Yesu kristo peke yake hivyo ni Vema tukajifunza kwake,
Mathayo
11:29 Jitieni
nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo;
nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.
Ø
Utu
wema
Ø
Upole
Ø
Unyenyekevu
wa Moyo
Ø
Kupata
raha nasfsini tunajifunza kwa Yesu
kristo,
Ø
Mungu
anataka ujifunze leo itakusaidika ikiwa utakuwa tayari kujifunza,
Ø
utayari
wako ni wa muhimu Sana ruhusu mabadiliko
yaanzie kwako,leo
Watu wengi sana
wanaokosewa Wanasamehe sana lakini
kusahau tukio au kwazo lililosababisha msaha utoke ni vigumu sana kusahau, Na hili ndilo jambo
linalowatesa kila inapoitwa leo,
kutosahau kosa baada ya kusamehe nikuendelea kuutunza Ugonjwa badala ya kutibu, Hata kanuni ya Mungu anaanza
kutusamehe kabla hajatuponya magonywa yetu,
Maandiko matakatifu yanatufundisha nini juu ya msamaha
Zaburi 103:3 Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa
yako yote,
4Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema,
5 Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;
6 Bwana ndiye afanyaye mambo ya haki, Na hukumu kwa wote wanaoonewa
4Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema,
5 Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;
6 Bwana ndiye afanyaye mambo ya haki, Na hukumu kwa wote wanaoonewa
Hakuna
mtu anayeweza kupokea uponyeji kutoka kwa Mungu kama hajasamehewa kwanza maovu
aliyoyatenda , Haijalisi umemkosea nani lakini kwakuwa ni uovu uliomchukiza
Mungu unahitaji kusamehewa au kusamehe na kusahau ili uwezekuponywa,
Madhara ya kimwili yanayosababishwa na kuto
kusamehe na kusahau
v Upweke
v Sura kupoteza Mvuto
v Kuto mwamini Mungu,kuto kuhudhuria ibada
v Kutokutoa kwaajili ya Mungu/
v kutokutunza familia
v kutojijali kimwil wewe mwenyewe
v Hamu ya kula inaweza ikapotea
v Manung’uniko kila wakati kwa kila jambo
unalofanyiwa
v Kutomwamini mtu yeyote,
v Unaweza ukasababisha Msongo wa Mawazo na ukajikuta
unaongea peke yako
v Unaweza kukonda sana au kunenepa kupita kawaida,
v Unaweza kupoteza ujasiri wa kila jambo
unalolifanya
v Unaweza kuwa Mubishi wa kila jambo, na mengineyo
mengi,
v Roho ya Maombi kutokuwepo
Ø Ukiomba Maombi yako hayatajibiwa,
Ø Uzee wako hautashibishwa siku wala mema
Ø Ujana wako hautaufurahia maana hautarejeshwa ,
Ø Kutokusamehe kunaambatana na Roho ya mauti,
Unahitaji Mema na
usalama jifunze kusamehe na kusahau,
Kwanini Ujifunze kusamehe na kusahau,
Unajifunza kusamehe kwa
sababu ulivyoumbwa asili yako si
uovu,wala mabaya bali asili yako ni mema
,upendo unaotokana na Mungu kwakuwa
Kuzaliana ni amri iliyoagizwa na
Mungu
Hivyo ikiwa asili yetu ni
upendo na Furaha ya Mungu mateso chuki Maovu yanatoka wapi ni kwa yule Muovu,
kupitia Wazazi,jamii mazingira , sasa katika hayo yametufarakanisha na Mpango
mzima wa Mungu, Mungu anataka akusamehe
leo na kukuponya kabla ya maombi jiulize swali hili uko tayari kusamehe,
Maandiko Matakatifu yanatufundisha nini juu
ya kusamehe?
Mathayo 6:14-15
Kwa
maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.
Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa
yenu.
Kumbe tunasamehewa
na Mungu Makosa yetu pale
tunapokuwa tayari kusamehe waliyotukosea, bila kuzingatia kosa walilolitenda
juu yetu, ni Hatari kubwa sana kutosamehe wanaotukosea,
kuto kusamehe
Kunaruhusu Roho ya mauti katika maisha
yetu,Biashara,Masomo,uchumba,ndoa,Huduma, na mengineyo mengi, Jifunze
leo,kusamehe na kusahau,
Warumi 6:23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama
ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
kumbuka Mungu alitusamehe
tangu awli kwa dhambi tulizotenda au kutendeshwa mwanzo kwakuwa malipo ya
Dhambi tulizokuwa tumefanya tulitakiwa kulipwa kifo,
ila kwa Neema ya Mungu
akakubali kulipa deni langu na lako, yeye ili sisi tuishi, swali la kujiuliza kwanini
unaishi, wengine unakuta anaomba kuongezwa miaka mingi umewahi kujiuliza Unaomba
Uishi miaka mingapi na ya nini, kwa sababu gani,
Maana kama utaishi Miaka
mingi kwa kumtumikia shetani utakuwa
umemchukiza Mungu sana hivyo utaishi
miaaka mingi ya Laana, ila ukimtumikia Mungu utaishi Miaka mingi ya Baraka,
chaguwa leo baraka,au laana mbele yako Mimi ninakushahuri samehe leo na usahau
kama uliwahi kutendewa hilo kosa,
Pamoja na Mateso yote aibu ya
kila namna Bado yesu akasema Baba Uwasamehe kwakuwa Hawajui watendala , Luka 23:34a
Sifa za Mwenye Kusamehe
Mtu mwenye uwezo wa kusamehe
ni yule Mtu aliyekubali Yesu akawa Bwana na Mwokozi wake Yaani (Aliyeokoka)
siyo anayejiita ameokoka maana uwezo
wakusamehe tunaupata ndani ya Yesu kristo, kipimo cha kujuwa kuwa huyu mtu
ameokolewa au bado ni kuangalia kama anauwezo wa kusamehe,na kusahau
Maandiko Matakatifu
yanatuhakikishia uwezo wa kusamehe unatoka kwa Mungu pekee,
Isaya 43:25 Mimi,
naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala
sitazikumbuka dhambi zako
Unapotubu kwa makosa
uliyoyafanya hakikisha wewe umeshawasamehe maana Mungu akisha futa makosa yako
hakukumbushii tena vinginevyo tungekumbushiwa tungekimbiana,
Waibrania 8:12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na
dhambi zao sitazikumbuka tena,Tatizo au kizuwizi kikubwa kinachotuzuwia Sisi kusikia au kuuona uwepo wa Mungu katika
Maisha yetu au katika kanisa la leo Hatujawa tayari kulipa Gharama ya Msamaha
Tunatamka kusamehe ila bado hatujakubali kulipa Gharama
ya kusmehe,
Gharama ya kusamehe ni kubwa Lakini ni lazima ilipwa,
ili kuwa huru kujipima kama
umefungwa au lah! Kipimo ni kujichunguza kama huwa unasame na kusahau,
Kusamehe kunahitaji gharama
ya kusahau Maana kutosahau kosa ni kidungo kwako na siku zote Mfungwa hana
maamuzi yake mwenyewe, hivyo ile dhambi itakutumikisha tu,
warumi 7;17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda
hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu
Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati.
Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati.
Kutofuta kosa ndani
ya moyo wako hauwezi kukuacha ukafanya unalotaka kulifanya ni sawa na
mtu anayedaiwa anakuwa hana uhuru kwakuwa wakati wote akimuona mdai anakumbuka
deni analodaiwa hata kama mdai hajaulizia Deni lake,
Hatari ya kutosamehe na kusahau,
Kutosamehe na kusahau
kutakusababishia kulipiza kisasi, mara nyingi watu wanaopenda kulipiza kisasi
ni wale watu wasiyoachilia maovu ndani ya miyoyo yao, kuka na kosa moyoni ni
sawana kujitegea Bomu ambalo Muda wowote linaweza kulipuka, na usipokuwa Makini
ukapata madhara hata wewe Mwenyewe, kuto kusamehe kunaambatana na Roho ya
Mauti, narudia tena bali kusamehe kunaambatana na Roho ya uzima,
Kukaa na tatiza moyoni ni
kama kujionganishia shoti ya umeme maana kila unapolikumbuka tatizo ulilokosewa
unaumia siku zote fahamu hili anayeumia siyo aliyekosa bali ni wewe uliyekosewa
kuwa Huru leo kwanzia sasa kwa kuanza kusamehe wote waliyokukosea, na jifunze
leo kusahau,usije ukalipiza kisasi,
Mambo ya walawi 19:18 Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana
wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi Bwana.
Kuwa na kinyongo ni kukaa na
Tatizo ndani ya moyo wako ambalo hutaki kuliachia juu ya mwenzako,
Kabila ya kufanya ibada ya Maombi hatua ya
kwanza ni kusamehe na kusahau
Marko
11:25 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili
na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
Kitu kinachofanya watu
waendelee kuteseka katika hali wanazopitia nikutofahamu kinachowaumiza ni yale
matatizo waliyoyashikilia ndani yao, japo katika nyumba za ibada wanaenda sadaka wanatoa kuimba wanaimba kusali wanasali
ila wanasali kwa bidii wakati hawajawa tayari kusamehe na kusahau,
Sasa wanapotoka katika ibada
tatizo linabaki pale pale,
Madhara ya ki-Roho Ya kuto samehe na kusahau,
Ø Kuto samehe ni kujifunga wewe mwenyewe kifungo asichoweza
mtu mwingine kukufunguwa na kisichojulikana mwisho
Ø Kuto kusamehe kuna kunyima msamaha wa Mungu
Ø Kutokusamehe kunakucheleweshea baraka zako,
Ø Kuto kusamehe kunakuongezea kukosea zaidi
Ø Kuto kusamehe kunatesa nafsi sana
Ø Kuto kusamehe kuna kutenga na Mungu
Ø Kuto kusamehe kuna kutenga na jamii ya Mungu
Ø Kunaweza kukukosesha Mbingu
Ø Kuto kusamehe kunaweza kukubadilishia hatima yako
bila kutarajia
Ø Kuto kusamehe kunakunyima uwezo wa kukuwa ki-Roho
au ki Huduma
Ø Kuto kusamehe kunakunyima kibali mbele za wengine,
Ø Kuto kusamehe kunaweza kukusababishia madhara ya
kimwili pia
Ø Kunaweza kukuondolea upendo(mathayo 24:12)Na kwasababu ya kuongezeka maasi upendo wa wengi
utapoa
v Unaweza kukosa Roho ya huruma kabisa
v Unaweza kuwa Mchoyo kabisa, unaweza kufa ki-mwili
na kiroho,
Waefeso
4:32 Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na
Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi. -
Hitaji kuu la kanisa la leo
ni kusamehe na kusahau
Mateso makubwa yanayotesa
kanisa la leo ni ile Roho ya kuto samehe na kusahau huu umegeuka kuwa Mtihani kwa watu wa Mungu,
iwe kwa waamini au wasiyoamini mtihani huu
umewaangusha watu wengi sana unawafelisha watu wengi sana, bila kuiangalia
kiwango cha kumjuwa Mungu, jifunze leo kusamehe na kusahau,
Nchi na Nchi zinapigana
kwaajili ya kuto kukubali suluhu ya kusamehana na kusahau,
Watu wangine wamefungwa bila
hatia kwasababu ya roho ya kisasi,watu wamenyimwa madaraka, wametengwa
makanisani,katika huduma,watumishi kwa watumishi, matajiri kwa masikini
Majumba ya ibada ni hivyo
hivyo Malumbano kila kukicha Malumbano hayo yote ni kuto kusamehana na kusahau
Wanandoa watateseka sana kinacho watesa niyalemakosa yaliyopita siyo
ya leo yaliyotendeka leo ni sababu tu, jifunze kusamehe na kusahau Ndoa yako
itakuwa salama yote hayo ni kuto samehana na kusahau, watoto kwa wazazi kutosamehana na kusahau
Kumewafarakanisha katika
jamii, kupotezana, kutokusaidiana kutokuheshimiana,
Majirani jamii nzima
kusameheana na kusahau, kumekuwa shida Dua yangu na Maombi Mungu atusaidie
Sana,
Tufanye nini ili kusamehe na kusahau
Kwa kuwa si Mpango wa Mungu
kuweka kisasi basi hayo yote tusimwangalie
Mwanadamu kama adui katika liletunalotendewa, Bali tumwangalie Muovu kwa
Macho ya Rohoni, na tufahamu kuwa Kila uovu unaotendeka Malengo makubwa ya
ibilisi ni kutuangamiza tu,
Hosea 4:6 watu wangu wanaangamizwa kwa
kukosa maarifa mithali 1:7 kumcha Mungu ni Chanzo cha maarifa
Wimbo ulio Bora 8:7 Dawa ya
haya yote ni Upendo maana upendo hauhesabu maovu, pia maandiko
yanatufundisha hata Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito
haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo
Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa.(kuchekwa)
Watu wengi wanapenda kuuongelea upendo sana hata mara nyingine kufundisha ila anapokosewa upendo unayayuka ghafla kutamka kinywani neno lolote ni Rahisi sana, tena sana kazi kuliishi lile unalolinena,
Watu wengi wanapenda kuuongelea upendo sana hata mara nyingine kufundisha ila anapokosewa upendo unayayuka ghafla kutamka kinywani neno lolote ni Rahisi sana, tena sana kazi kuliishi lile unalolinena,
1wakorintho 13:1 Nijaposema kwa lugha za
wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa
shaba iliayo na upatu uvumao.
Kutokusamehe na kusahau ni Roho ambayo inaweza
kukaribisha Maroho Mengine mabaya zaidi na ili yakuuwe, yohana 10:10
kutokusamehe kunafunguwa mlango wa kuibiwa,kuchinjwa,kuharibiwa mali kuuwawa,
shugulikia Roho ya kuto samehe na kusahau, roho ya mashitaka futa,
Hitimisho
Maombi:
Baba ninaomba uniponye na matatizo
yaliyoingia ndani yangu kwasababu ya kutokusamehe na kusahau katika Jina la Yesu. Leo ninabadilika katika
Jina la Yesu. Mimi ni mzima na nimeponywa katika Jina la Yesu…..
Futa hati zote za mashitaka, alizotunza Ibilisi, ili
usijekukumbushiwa na Ibilisi mengine tena
Ufunuo
12:10. "Nikasikia sauti kuu mbinguni,
ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya
Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye
mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. Nao
wakamshinda kwa Damu ya Mwanakondoo na kwa Neno la ushuhuda
wao, ambao hawakupenda Maisha yao hata kufa,
Baba katika jina la Yesu ninafuta
mashitaka yote yaliyoandikwa dhidi yangu, familia, biashara, uchumba,
elimu,kazi, kwa Damu ya Mwanao wapekee Yesu kristo kila shitaka lililokuwa limeifadhiwa Makitaba
ya Ibilisi ninaifuta sasa hivi, katika jina la yesu,
1Petro
1:10
Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa
Utawanyiko, wakaao hali ya ugeni katika Ponto, na Galatia, na Kapadokia, na
Asia, na Bithinia;
2 kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika kutakaswa na Roho, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu.
2 kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika kutakaswa na Roho, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu.
3 Ahimidiwe
Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa
mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo
katika wafu;
4 tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.
4 tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.
5 Nanyi
mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari
kufunuliwa wakati wa mwisho.
6 Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;
7 ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.
6 Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;
7 ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.
8 Naye
mwampenda, ijapokuwa hamkumwona; ambaye ijapokuwa hamwoni sasa, mnamwamini; na
kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu,
9 katika kuupokea mwisho wa imani yenu, yaani, wokovu wa roho zenu.
10 Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza, ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi.
9 katika kuupokea mwisho wa imani yenu, yaani, wokovu wa roho zenu.
10 Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza, ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi.
Somo hili ni maalumu maishani mwako pata DVD,CD,VCD, Utasaidika sana piga
0756 809 209 au 0653 29 42 19
Ila kuishinda Roho hii ni kuomba Mungu akupe Roho ya
upendo
1wakoritho 13:4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo
hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
Tufanye nini ili kuweza kusamehe na kusahau,
Nirahisi sana jichunguze Moyoni mwako yupo nani yupo
muovu iblisi au Bwana yesu, ikiwa ndani yupo kristo Yesu yeye ni msingi wa
upendo andoa shaka, omaba sasa kupitia Roho Mtakatifu akusaidie kukusanya kila
ubaya wa Namna zote uliyokuwa umerundikana ukakusababishia kuto samehe
,waefeso 3:17 Kristo akae mioyoni mwenu kwa
imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;
Hitimisho kwaajili ya wewe kuwa salama Baada ya kufanya
sala ya toba maagizo Maalimu toka kwa bwana Mungu
Kumbu kumbu la Torati 6:5,11:1,mathayo
22:37 ,Marko 12;31,Luka 10:27 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa
roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
Yote ya yote Maagizo aliyoyaagiza Bwana yesu ambayo leo
kanisa limeyaacha kabisa ni haya maagizo
hapa,
Mathayo 5:44,mathayo 10:36 , lakini mimi
nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni
wanaowaudhi,
sasa nakuomba
sasa nakuomba
Mathayo 13;25 lakini watu walipolala, akaja
adui yake akapanda magugu katikati ya ngano,
akaenda zake.
Anza kushugulikia pando ambalo hakulipanda Baba wa Mbinguni na uanze pia kusamehe na kusahau kisha uanze kuombea Adui zako Masamaha pia
Anza kushugulikia pando ambalo hakulipanda Baba wa Mbinguni na uanze pia kusamehe na kusahau kisha uanze kuombea Adui zako Masamaha pia
Wahoo somo Hili linapatikana pia katika
DVD,VCD,CD
Yapo masomo mengine mengi yanayokufaa sana,
Ukihitaji Masomo mengine agiza utayapata,
v Siri kuu tatu za kutuza siri zako
v Upenyo wa kumiliki
v Nguvu ya kinywa
v Hatima iliyopindishwa
v Ushindi katikati ya vita
v Jifunze kusamehe na kusahau na mengineyo mengi, pia utapohitaji ushahuri au maombi umbali usikuzuwie kuhudumiwa piga simu kisha utapata nafasi ya kuongea live na Mtu wa Mungu Nabii Samson, piga sasa ni bure 0756 809 209 .0653 29 42 19

Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12
Comments