Unajua kuna watu ambao huwa wanajilaumu kwa naman ambavyo wapo, kuna waschana wengine wanapowaona waschana wenzao ni wazuri zaidi yao basi hujiona kuwa wao hawastahili kabisa, kuwaepo katika ulimwengu wa Warembo, nipende kukuasa wewe Binti ambaye umeumbwa ukiwa na sura mbaya, mshukuru Mungu kwa kukuumba hivyo, maana amekuepusha na mambo mengi ambayo yangekunasa endapo tu kama ungepewa uzuri.
![]() |
Na Abel Suleiman Shiriwa |
2 Korintho 4:15 Kwa maana mambo yote ni kwa ajili yenu, ili neema hiyo
ikiongezwa sana, kwa hao walio wengi shukrani izidishwe, na Mungu
atukuzwe.
16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
17 Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana;
18 tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
Na wewe mwanamke mzuri umepewa uzuri huo na Mungu kwa makusudi maalumu ya kuipeleka kazi yake mbele, maana kama wewe uliye na sura nzuri Shepu nzuri, ukiweza kumtumikia Mungu ka kweli, utawafanya hata wale ambao wana sura mbaya, wajione kuwa wao si kitu kwa kutokumtumikia Mungu, kwani watajiuliza kama wewe mzuri ambaye unakutana na vishawishi vingi vya kukutoa katika utaratibu wa Mungu, na umeweza kuvishinda, sasa ni vipi wao wabaya washindwe kumtumikia Mungu? Uzuri wako utakuwa ni moja ya kivituo kwa watu kuja kumtumikia Mungu kwa kweli, maana wengi hudhani binti mzuri hawezi kuwa mcha Mungu….. hivyo utumie uzuri wako kwa kazi ya Mungu, maana utakuja daiwa siku ile iliyo kuu siku ambayo watu tutakimbiana siku ambayo usiitamani kuikuta kwa wewe mwenye dhambi
By Abel Suleiman Shiriwa
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12
16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
17 Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana;
18 tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
Na wewe mwanamke mzuri umepewa uzuri huo na Mungu kwa makusudi maalumu ya kuipeleka kazi yake mbele, maana kama wewe uliye na sura nzuri Shepu nzuri, ukiweza kumtumikia Mungu ka kweli, utawafanya hata wale ambao wana sura mbaya, wajione kuwa wao si kitu kwa kutokumtumikia Mungu, kwani watajiuliza kama wewe mzuri ambaye unakutana na vishawishi vingi vya kukutoa katika utaratibu wa Mungu, na umeweza kuvishinda, sasa ni vipi wao wabaya washindwe kumtumikia Mungu? Uzuri wako utakuwa ni moja ya kivituo kwa watu kuja kumtumikia Mungu kwa kweli, maana wengi hudhani binti mzuri hawezi kuwa mcha Mungu….. hivyo utumie uzuri wako kwa kazi ya Mungu, maana utakuja daiwa siku ile iliyo kuu siku ambayo watu tutakimbiana siku ambayo usiitamani kuikuta kwa wewe mwenye dhambi
By Abel Suleiman Shiriwa
Comments