![]() |
Askofu Kakobe |
Kupitia tukio hilo, askofu Zachary Kakobe wa kanisa la Full Gospel Bible
Fellowship pamoja na askofu Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na
Uzima wanatarajiwa kufundisha masomo tofauti ili kuwaweka sawa watu
watakaohudhuria tukio hilo kabla ya kuingia kwenye kipindi cha maombi
kwa Taifa. Viongozi wengine ni pamoja na mwenyekiti wa baraza la
makanisa ya kipentekoste nchini askofu David Batenzi pamoja na katibu
wake askofu David Mwasota wa Naioth Gospel Assembly na viongozi wengine
wa makanisa ya Kiroho wanatarajiwa kuwepo siku ya leo.
Kwa taarifa hii mabayo mwenyekiti wa baraza la makanisa ya kipentekoste
mjini Dar es Salaam, askofu Bruno Mwakibolwa, waamini wanatakiwa kufika
kuanzia saa tatu asubuhi, na kisha ratiba ya mafundisho na kisha
kuendelea na maombi, ikiwa ni siku ya hitimisho katika siku 40 ya maombi
yalioanza mnamo Januari 6 2014.
Na Gospel kitaa
Comments