MAOMBI YA KWELI NI USHIRIKA NA MUNGU




 
BWANA YESU asifiwe ndugu
Karibu katika fundisho hili muhimu linalohusu maombi.
1 Thesalonike 5:17-18. ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya MUNGU kwenu katika KRISTO YESU.
Maombi ni muhimu sana kwa kila mwamini.
Yeremia 17:14.Uniponye, Ee BWANA, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu.
 
Maombi ni mahitaji ambayo mwanadamu anapeleka kwa muumba wake.
Maombi ni maneno maalumu anayoyatamka mwamini kwa imani ili yaende kwa muumba wake, ambaye siku zote yuko tayari kujibu maombi.
Maombi ni maisha ya mwamini.
Zaburi 27:8.Uliposema, Nitafuteni uso wangu, Moyo wangu umekuambia, BWANA, uso wako nitautafuta. 

Maombi ni njia ya mawasiliano kati ya MUNGU  na watoto wake waliosafishwa kwa damu ya mwanawe wa pekee YESU KRISTO.

Maombi ndio mawasiliano kati yetu wanadamu na MUNGU Baba yetu.

Ili uhusiano wetu na MUNGU uwe hai  lazima tuwe waombaji.
Zaburi 62:8. Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; MUNGU ndiye kimbilio letu.

MUNGU huongea na sisi kwa njia ya neno lake kupitia kusoma kwetu Biblia na huongea na sisi kupitia watumishi wake, na sisi tunaongea na MUNGU kwa njia ya maombi, hivyo ili uhusiano wetu na MUNGU uwepo lazima tuwe na muda wa maombi.

KUNA MAOMBI YA AINA  NYINGI.
Wakolosai 4:2.Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani;

tusome pia Yakobo 1:5.Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa MUNGU, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.

1:    Maombi ya shukrani.-   Tunamshukuru MUNGU na kumrudishia heshima kwa aliyo yafanya kwetu. Mfano ametulinda, ametuokoa n.k

2:   Maombi ya kusihi-     Tunamsihi MUNGU juu ya jambo Fulani tunalolihitaji, mfano MUNGU aponye nchi yetu, awafungue ndugu zetu waliofungwa na dhambi au mambo mengine.

3:   Maombi ya kuomboleza-  unaomboleza juu ya jambo baya lililokupata mfano ukimwi, au motto wako kupatwa na kichaa n.k

4:   Maombi ya toba. -  Haya ni muhimu sana na ni ya kwanza kabisa maana kutubu kwanza ndilo jambo la muhimu sana kwa kila mwanamaombi. Kutubu ndio kumruhusu MUNGU ashughurike na mahitaji yako. Maombi ni unyenyekevu.

5:  Maombi ya vita: -  Haya ndio maombi muhimu zaidi, hata kama maombi yote ni muhimu sana. Hapa unatumia mamlaka ya KRISTO iliyoko ndani yako kuharibu mipango ya shetani juu ya maisha yako. N.k. 

6:    Maombi ya kufunga: -  Unafunga kuombea jambo Fulani na wakati wa kufunga unaweza ukahusika na aina zote za maombi hapo juu.

Zaburi 34:4. Nalimtafuta BWANA akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote. 

-Aina zote za maombi ni muhimu sana, na kwa kuomba maombi ya kweli  ndio uhusiano wako na MUNGU  unakua mzuri zaidi.

-Yapo mambo mengi ukiyafanya yatakuweka katika uhusiano mzuri na MUNGU katika KRISTO. Mfano kumtumikia, utakatifu, kumtii ROHO MTAKATIFU lakini mimi najua ya kwamba haiwezekani kuyatimiza hayo yote bila kuwa mtu wa maombi, hivyo maombi ni muhimu sana.

Zaburi 66:20. MUNGU kwetu sisi ni MUNGU wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA BWANA.

Sio kila maombi yanajibiwa na sio kila mtu ana sifa za kuomba na akajibiwa.

Sifa ya mwombaji anayeweza akaomba na akajibiwa ni kwanza kumpa BWANA YESU KRISTO maisha yako, na kufanya toba ya kweli na kukaa ndani ya KRISTO. Yeye anasema hivi katika Yohana 15:7 . Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa. 

Tena waliompokea BWANA YESU yeye aliwafanya kuwa watoto  wa MUNGU ndio wale waliaminio jina lake(Yohana 1:12)

Tuombe katika jina la YESU KRISTO.

Tuombe katika ROHO MTAKATIFU.

Tuombe kwa imani 

Tuombe maana MUNGU hujibu maombi.

Tena BWANA YESU anasema katikaYohana 14:14.kiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya. 

 Kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                 MUNGU akubariki sana .
                  Ni mimi ndugu yako
                  Peter M Mabula
         Maisha ya Ushindi Ministry.
                   0714252292

Comments