MAOMBI ZAIDI KWA DARLENE, KANSA YASABABISHA NYWELE ZAKE KUANZA KUNYONYOKA

Darlene Zschech katika moja ya huduma zake ©screen grab/youtube.
Maombi zaidi ya uponyaji yanahitajika kwa mwanamama Darlene Zschech ambaye alikuwa kiongozi wa bendi ya kanisa la Hillsong Australia kabla hajaama na kuanza kutunza kanisa lake na mumewe Mark liitwalo Hope Unlimited kwakuwa tangu agundulike kuwa na kansa ya maziwa mwishoni mwa mwaka jana, mwanamama huyo ameanza kupoteza nywele zake ambazo zinanyonyoka ikiwa ni awamu ya kwanza ya matibabu ya mionzi kuukabili ugonjwa huo.

Darlene na mumewe Mark.
Kwa mujibu wa taarifa yake aliyoitoa kwa mashabiki na watu wanaomuombea kupita salama katika jaribu analopitia hivi sasa, mwanamama huyo amesema licha ya kugundua kunyonyoka kwa nywele zake bado hajakata tamaa ya kumuamini Mungu ikiwa pamoja na hamu yake ya kumuabudu Mungu bado imeujaza moyo wake na kwamba anachohitaji ni neema tu ya Mungu, kwakuwa amejifunza kumtegemea na katika ahadi zake. Mwanamama huyo amesema tangu agundulike kuwa na ugonjwa huo amepata wasaa wa kuandika nyimbo zaidi na kwamba amepanga mwezi November mwaka huu kufanya ibada ya shukrani ambayo itaambatana na kushirikisha watu nyimbo na hisia zake pindi Mungu atakapomvusha salama mpaka ng'ambo nyingine kutoka katika matatizo aliyonayo kwasasa.

                               Gospel kitaa


Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments