Mwaliko wa mbinguni ni muhimu sana kwa kila mtu kuuitikia.

BWANA YESU asifiwe leo tuangalie mwaliko wa kwenda mbinguni.

Mialiko yote hushtusha sana na kuamsha hamasa kubwa.
Twajisikia ya kwamba ni ya muhimu sana, pia yatuhamasisha
kweli. Kwa maana hiyo basi, tuitikie na mwaliko huo wa
kwenda  mbinguni kwa sala fupi kama ifuatavyo:

»BWANA YESU, nimeishi hadi leo kama wewe

haupo. Nimetambua sasa, wewe u nani na kwa saba-

bu hiyo naja kwako mara ya kwanza kwa sala. Najua

sasa ya kwamba kuna Mbingu na Jahanamu. Niokoe

na jahanamu, mahali ambapo kwa dhambi yangu na

kutoamini kwangu ningestahili kwenda. Ni hamu yangu,

kuwa pamoja nawe mbinguni milele. Najua ya kwamba

siwezi kufika mbinguni kwa matendo yangu mazuri,

bali kwa kukuamini wewe. Kwa sababu wewe hunipen-

da ukanifia msalabani na kubeba makosa yangu yote

na kunilipia. Nakushukuru kwa hayo. Waona dhambi

zangu, hata yale yote kuanzia ujana wangu. Kila dham-

bi mojamoja ya maisha yangu waijua – yote ninayo-

kumbuka na zile ambazo nalisahau. Wewe wanijua

kabisa. Waelewa hisia zote za moyo wangu, ikiwa ni

furaha au masikitiko, ustawi au kukata tamaa. Mimi

ni kama kitabu kilicho wazi mbele yako. Jinsi nilivyo

na jinsi maisha yangu yalivyo hadi sasa, siwezi kuis-hi nawe na MUNGU aliye hai na ningestahili kuikosa

mbingu. Kwa hiyo nakusihi, unisamehe dhambi zangu

zote. Nasikitika kwa ajili ya dhambi zangu. Tafadhali,

nisaidie kuvua yote yasiyo sawa mbele zako na unipatie

uadilifu unaoniwezesha kuishi chini ya baraka zako.

Nifungulie uelewo wa Neno lako la Biblia. Nisaidie

kuelewa unachotaka kuniambia, ili nipate nguvu mpya

na furaha ya maisha kutoka katika Neno lako. Wewe

ni BWANA wangu kuanzia sasa. Mimi ni mali yako na

ninataka kukufuata. Unionyeshe njia ambayo naweza

kwenda. Nakushukuru kwamba umenisikia. Naamini

ahadi yako ya kwamba kwa kukugeukia nimepata kuwa

mtoto wa MUNGU, ambaye atakuwa pamoja nawe mbin-

guni milele. Nafurahi sana kujua, mimi ni pamoja nawe

na wewe u kwa kila hali upande

wangu. Nisaidie kukutana na watu

wanaokuamini na niweze kushiri-

ki katika kanisa ambapo naweza

kupata kusikia na kulishwa Neno

lako daima. Amina.«

MUNGU akubariki sana na kwa ushauri na maombezi wasiliana nami kwa namba 0714252292.
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.

Maisha ya ushindi ministry


 

 Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments