Kanisa la kwanza lilihubiri
Wokovu na watu Waliamini na Kuokolewa. Baada ya watu Kuamini Habari
Njema ya Injili ya Yesu Kristo, watu Walibatizwa na kufanyika wanafunzi
wa Yesu na kujiunga na wanafunzi wengine na kwa jinsi hiyo Kanisa
liliongezeka. Kanisa la kwanza lilitembea katika Huduma (vipawa) zote
Tano (Mitume, Manabii, Wainjilisti, Walimu na Wachungaji), Huduma zote
Tano zilikuwepo. Kanisa la kwanza lilitembea katika Karama zote Tisa za
Roho Mtakatifu, bila kubagua hata karama mojawapo na kutengeneza
visingizio. Kanisa la kwanza lilitembea katika kutenda kazi zote. Kanisa
la kwanza lilifanya sawasawa na Agizo
la Bwana la kuhubiri Injili kwa kila kiumbe, Injili AMBAYO NI UWEZA WA
NGUVU UULETAO WOKOVU KWA KILA AAMINIYE, na kisha kufundisha yale
aliyoamuru Bwana Yesu. Kanisa la kwanza lilibatiza baada ya mtu kuamini
Ujumbe wa Injili iletayo Wokovu kwake yeye aaminiye na kufanyika
mwanafunzi, na kwa ubatizo huo, huyo mtu alikuwa anakiri kile
alichoamini, na hivyo kufanyika kUwa wa YESU KRISTO. Kanisa la kwanza
lilitembea katika Ishara zote alizosema Bwana Yesu kuwa wale wamwaminio
wataambatana nazo na wala hakukuwa na longolongo. KAZI, HUDUMA, KARAMA,
NA ISHARA VILITEMBEA NA KANISA LA KWANZA. LEO KUNA WAZIMU GANI NA UPUUZI
GANI UNAENDELEA KATIKA MADHEHEBU YA KIKRISTO? JE HAYA MAMBO YAPO? NA
KAMA YAPO JE YAPO KWA KIWANGO GANI? NA KAMA HAKUNA, JE NI NINI SABABU YA
KUTOKUWEPO? DHEHEBU GANI LA KIKRISTO LEO LINAWEZA KUJILINGANISHA NA
MTEMBEO WA KANISA LA KWANZA? NA KUSEMA LIKO KATIKA RAILTRACKS IZIPASAYO
KANISA LA YESU KRISTO? ULE MWILI WA KRISTO AMBAO YESU ALIMUULIZA SAUL
SAUL KWANINI UNANITESA....NI DHEHEBU GANI LEO LINA UJASIRI WA KUSEMA
SISI NDIO WENYEWE? KWA KUJIFANANISHA NA MTEMBEO WA KANISA LA KWANZA, LA
WALE WANAFUNZI WALIOITWA WAKRISTO PALE ANTIOKIA, NA TENA WAKAITWA WATU
WA MADHEHEBU YA WANAZORAYO, HUKU MTUME PAULO AKINENWA KUWA KIONGOZI
WAO....NI DHEHEBU GANI LA KIKRISTO LEO LINA UJASIRI? UJASIRI WA KUWEKA
KELELE ZA MAFUNDISHO YAKE PEMBENI NA KUSEMA SISI NI KAMA WALE WA KANISA
LA KWANZA, KWA KAZI LIFANYAZO, HUDUMA TANO NDANI YAKE, KARAMA TISA ZA
ROHO MTAKATIFU NA UDHIHIRISHO WA ISHARA ALIZOSEMA BWANA YESU...NI
DHEHEBU GANI LEO? By Sam Balele
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12
Comments