UKUMBI WA PTA WARINDIMA KWA MAOMBEZI YALIYOFANYWA NA WAPENTEKOSTE KWA TAIFA

Siku ya jana ndani ya ukumbi wa PTA uliopo ndani ya viwanja vya maonyesho vya mwalimu JK Nyerere almaarufu kama Sabasaba kulifanyika maombi maalumu kwa Taifa yakiongozwa na umoja wa makanisa ya Kipentekoste nchini. Katika maombi hayo yaliyohudhuriwa na waumini lukuki sambamba na wachungaji wao ilishuhudia askofu Zachary Kakobe pamoja na Josephat Gwajima wakiongoza maelfu ya waumini waliofika ukumbini hapo katika kuhubiri neno la Mungu kwa ufupi kisha kuingia katika maombi ambayo yaliandaliwa vyema na umoja huo.















                                                          Kwa hisani ya Gospel kitaa

Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments