YESU ANAKUJA, UWE TAYARI.



           
         


BWANA YESU asifiwe.
Ni neema ya MUNGU kwamba tuko salama, ni makusudi ya MUNGU tuendelee kuishi katika Mwana wa pendo lake, BWANA wetu YESU KRISTO.

Lengo kuu la somo hili ninalokuletea mwana maisha ya ushindi mwenzangu ni kuwa tayari kwa ujio wa BWANA YESU , ambapo wanadamu wote wanautarajia ujio huo.
Hakuna ajuaye siku wala saa ila BWANA MUNGU mwenyewe, lakini kuwa tayari ni jukumu la kila mwanadamu.
1 Thesalonike 4:16-17.( Kwa sababu BWANA mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya MUNGU; nao waliokufa katika KRISTO watafufuliwa kwanza.  Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki BWANA  hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na BWANA milele.   )

BWANA YESU aliianzisha kazi hii muhimu ya kutufanya tuurithi uzima wa milele, na siku moja atakuja kuimaliza ili waliotii wapate nafasi ya kufurahi na BWANA milele.
Yakobo 5:8-9(Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake BWANA kunakaribia. Ndugu, msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.  ).

                            KWANINI TUWE TAYARI KILA SAA?


Biblia haijachagua kwamba tujitahidi kuwa tayari, kila mwaka, au kila mwezi  au kila wiki, wala Biblia haisemi kwamba tuwe tayari siku furahi tu bali kila saa inayotokea maishani mwetu.
Tuwe tayari mpendwa, tuwe tayari maana tunaishi katika nyakati mbaya sana.

       SABABU 7 ZA KWANINI TUWE TAYARI KILA SAA KWA UJIO WA BWANA YESU.

1. Kwa sababu hatujui siku wala saa ya kuja BWANA.(Luka 12:40-Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.)

2. Kwa sababu dalili zote za siku za mwisho zimekwishatokea.(2 Timotheo 3:1-7-Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,  wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,  wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda MUNGU;  wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.  Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi; wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.)

3. Kwa sababu BWANA YESU anatuandalia makao mbinguni na sisi hatutakiwi kukosa furaha hiyo ya milele  (Yohana 14:1-3-Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini MUNGU, niaminini na mimi.  Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.)

4. Kuna jehanamu ya moto kwa ambao hawakumpokea BWANA YESU kama BWANA na MWOKOZI wao kipindi wakiwa hai. 1 korintho 6:9-11-Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa MUNGU? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.  Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la BWANA YESU KRISTO, na katika Roho wa MUNGU wetu. , 

5. Kwa sababu tukishinda ya dunia  kuna furaha ya milele, Yohana 5:24-Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani., Wagalatia 6:8-Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. Hivyo tuutafute kwanza ufalme wa MUNGU Mathayo 6:33-Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa..

6. Maisha yajayo ya uzima wa milele, hakutakuwa na dhiki za dunia tena kama kifo, njaa, mateso, magonjwa au uonevu wowote. Ufunuo 22:3-5-Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha MUNGU na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia;  nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.  Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa BWANA MUNGU huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele.


7. Kwa sababu kila mtu atavuna alichopanda maishani mwake akiwa duniani/ kwa sababu kuna hukumu. Mathayo 13:49-50-Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,  na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.



Tumejifunza juu ya sababu za kuwa tayari  kwa siku ya BWANA,
Jambo jingine muhimu linatokea hapa. Yaani nini cha kufanya cha kufanya wakati wa kumngonjea BWANA YESU..


TUFANYENINI WAKATI WA UTAYARI WETU WA KUMNGOJEA BWANA YESU? 

2 Korintho 7:1- Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha MUNGU.

1.Tukae ndani ya YESU KRISTO 1 Yohana 2:28 -Na sasa, watoto wadogo, kaeni ndani yake, ili kusudi, atakapofunuliwa, mwe na ujasiri, wala msiaibike mbele zake katika kuja kwake..

2.Tujitakase na kuishi maisha matakatifu.

3. Tufanye kazi ya MUNGU.Wafilipi 2:13- Kwa maana ndiye MUNGU atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema..

4.Tuzae matunda mema kwa kuwaleta  watu kwa YESU.Yohana 15:16- Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo BABA kwa jina langu awapeni.

5.Tumwabudu MUNGU katika Roho na kweli.Yohana 4:24- MUNGU ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

6. Tuharibu ufalme wa shetani na tuujenge ufalme wa MUNGU. Yeremia 1:10- angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.

7.Tuitumie mamlaka ya KRISTO iliyoko ndani mwetu kuwaombea watu ili MUNGU awaponye na awatenge na kamba zote za shetani ziliwafunga. Yakobo 5:15-16- Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na BWANA atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa. Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii..

BWANA YESU asifiwe.
Tunapomngoja BWANA si kwamba  tutatakiwa kwenda sehemu fulani kusubiri, bali tunamsubiri BWANA huku tukiishi duniani na tunakuwa tunaendelea na Maisha kama kawaida, huku tukizingatia mambo hayo 7 hapo juu na kuyatenda tungali hai..
Wokovu ni sana ndugu, Wokovu si wa kukosa, BWANA YESU atarudi siku moja kuona umefanya nini katika maisha haya.
Kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                       MUNGU akubariki sana
                Ni mimi ndugu yako katika BWANA YESU.
                  Peter M Mabula
                 Maisha ya ushindi Ministry.
                               0714252292

Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments