GWIJI WA UCHAWI KWA MIAKA 80 AKABIDHI MIKOBA YAKE YA UCHAWI MKUTANO WA VHM BAGAMOYO

Mchungaji Peter Mitimingi akinyanyua juu mkoba wa uchawi wa babu  kwa makutano.
Huduma ya sauti ya matumaini ama The Voice of Hope Ministries (VHM) chini ya mkurugenzi wake mchungaji Peter Mitimingi imeendelea kumshinda shetani na kurudisha mateka kwa Yesu safari hii ikiwa katika moja ya vijiji wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Ambapo katika mkutano huo mmoja kati ya magwiji wa uchawi wilayani humo mwenye umri wa miaka 80 amekabidhi mfuko wake wa uchawi na kumpa Kristo maisha yake. Mzee huyo amesema amefanya shughuli za kichawi toka akiwa mtoto mdogo ambapo ameshindwa kukabidhi mtu wa kurithi mikoba hiyo kutokana nayeye kuwa mzee nguvu za mwili zinamuishia hali inayomfanya ashindwe kutimiza majukumu yake inavyotakiwa na kuwakasirisha majini yake ambayo humuangushia kipigo kutokana na ugoigoi wake.
Baada ya kusikia makomandoo wa Yesu VHM wapo kijijini kwake aliamua kwenda kuroga na kukutana na mzinga wa nguvu za Mungu na kujikuta akisalimisha mizigo yake yote ya uchawi kwa watumishi wa VHM ambao bado wanapiga injili kijijini hapo.

Huduma ya VHM imekuwa ikijishughulisha na injili sehemu za vijijini na mijini ambako kuna ugumu wa injili kufikika kwa urahisi hasa kutokana na sifa za kuwepo nguvu za kishirikina ama kutowahi kusikika injili kabisa na watu wamekuwa wakionewa na nguvu za giza. Ili kujua mengi kuhusu huduma hii ama kutaka kuchangia huduma hii ofisi zao zipo Mwenge jijini Dar es salaam karibu na hospitali ya mama Ngoma au wapigie simu ifuatayo 0713 183 939

Muhubiri wa mkutano huo mwinjilisti Lonas Khiwele akiunyanyua juu mkoba wa uchawi wa babu mbele za watu.
Mkoba ukiwekwa sawa kuchomwa moto.
Umati wa watu mkutanoni hapo. 


Wakati wa kumshambulia shetani.
Mfuko wa babu ukichomwa mbele ya umati wa watu.
Kwa Yesu ndiko kwenye usalama wa uhakika, umati ukikubali kumfuata Kristo.>>>>
CHANZO CHA HABARI GOSPEL KITAA ( GK

Comments