KANISA KATOLIKI NA MSIMAMO KUHUSU KATIBA MPYA

Kardinali Pengo ©ipp media
Akiweka bayana kuhusu maoni ambayo hawakubaliani nayo, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki jimbo kuu la Dar es Salaam, Kardinali Polycarp Pengo, amesema kuwa masuala ya kuoana mwanaume kwa mwanaume (ikiwemo mwanamke kwa mwanamke), au kuua wazee, au utoaji wa mimba, basi ni mambo ambayuo dhahiri hawatakubaliana nayo, ikiwa litakuwa kwenye Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Msimamo huu umewekwa bayana pale ambapo Kardinali Pengo alipokuwa akieleza msimamo wa Kanisa Katoliki kuhusu muundo wa serikali tatu, tofauti na kama ambavyo vyombo vya habari vilinukuu taarifa kutoka kwa Tume ya Haki ya Amani ya Baraza la Maaskofu (Katoliki) Tanzania ambapo walilitaka Bunge kutokashifu mapendekezo ya serikali tatu, kwani yataleta mshikamano zaidi.

Halikadhalika baraza hilo limesema katika tamko lake hilo kuwa kuna mambo yenye tija zaidi pia kwenye rasimu hii ya pili, na sio masuala ya muungano tu.

Kauli ya Mhadhama Kardinali Pengo inatofautiana na ile ya Tume ya Haki ya Amani ya Baraza la Maaskofu (Katoliki) Tanzania, ambapo ameweka bayana kuwa huo haukuwa msimamo wa Kanisa Katoliki, na kwamba ingeelezwa iwapo ingekuwa hivyo.


Rasimu ya kanuni za bunge maalumu la katiba ndio inaendelewa kujadiliwa, ambayo itatoa mwongozo namna ambavyo mjadala utakuwa na namna ya kufikia maamuzi kwa vifungu vya rasimu ya pili ya katiba, ambapo baada ya hapo kura za wananchi (walioandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura) ndio watakaoamua.
 
                     chanzo : Gospel kitaa

Comments