Mwanamke aliyefanyiwa
ukatili wa kijinsia kwa kukatwa mkono na sehemu za siri na anayedaiwa
kuwa mume wake, amepata msaada wa kuendeleza matibabu yake kutoka Kanisa
la Anglikana Jimbo la Mara kupitia kitengo cha maendeleo ya jamii.
Akizungumzia msaada huo, Meneja Mradi wa Maendeleo
ya Jamii wa kanisa hilo, Theophir Kayombo alisema kanisa limeamua
kumsaidia mama huyo baada ya kumsikia akitoa ushuhuda katika Maadhimisho
ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kimkoa yalifanyika wilayani Bunda.
Alisema kanisa liliguswa na ukatili aliofanyiwa
mama huyo kwa kufuatwa nyumbani kwake usiku akiwa na watoto wake na
kuanza kukatwa sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kayombo alisema mama huyo alikuwa katika matibabu
ambayo hata hivyo amepewa rufaa ya kwenda Hospitali ya (KCMC) Moshi kwa
matibabu zaidi na kwamba kanisa hilo la Anglikan kupitia ktengo chake
cha huduma na maendeleo kwa jamii litahakikisha linamgharimia mama huyo
hadi pale atakapopona tatizo hilo linalomsumbua.
Aidha aliiasa jamii kuhakikisha wanawakinga
wanawake na watoto wao na wananchi kwa jumla na vitendo vya ukatili wa
kijinsia ambavyo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikisababisha vifo kwa
wahusika, huku wengine wakibakia kupata ulemavu wa kudumu na hatimaye
kurudisha maendeleo ya jamii na Taifa kwa kushindwa kushiriki shughuli
za maendeleo na wengi kuwa maskini.
Comments