KANUNI 10 ZA VIJANA KUJIANDAA KABLA YA NDOA!


Na Mchungaji Peter Mitimingi

1. Jifanyie Maboresho wewe Mwenyewe yaani Imrove yourself.

2. Anza kujifunza sifa juu ya mume mzuri yukoje na Mke mzuri yukoje.


3. Tafuta kujua Baba mzuri anakuwaje au mama mzuri anakuwaje.
4. Jifunze kuwa mkomavu sio kudeka deka kwa vitu vidogo unataka mpaka wazazi wakufanyie. Mfano kuna baadhi ya vijana ni "MIJEBA" lakini bado wanaomba pesa za kunyolea ndevu kutoka kwa wazazi wao halafu unataka kuwa mume..


5. Jitahidi kuhudhuria mafunzo mbalimbali juu ya mambo ya kabla ya ndoa "pre-marital trainings, seminars.


6. Soma vitabu mbalimbali vya mambo yahusuyo namna ya kuingia kwenye ndoa.


7. Sikiliza vipindi vya vyombo vya habari vinavyofundisha mambo yahusuyo kuingia kwenye ndoa.


8. Jifunze mambo Mema na uyafuate na usitafute mifano ya walioshindwa katika ndoa zao kama nguzo ya kuegemea.


9. Rudisha Tabia njema za zamani ulizoziacha.


10. Epuka misimamo migumu na isiyo ya msingi ya kimila au kimakabila zingatia nyakati na utakatifu.

Comments