MANENO YANAYOTOKA KWENYE KINYWA CHA MTUMISHI WA MUNGU.




BWANA YESU KRISTO apewe sifa ndugu zangu.


Ni siku nyingine nzuri aliyoifanya BWANA, ambapo tunakutana hapa ili tujifunze neno la MUNGU.

Namshukuru sana MUNGU kwa kunipa ujumbe huu mzuri wa kulifaa kanisa lake kokote duniani.


Karibu.


Maneno hutoka katika kinywa.

Kinywa kinaumba.


Unaweza ukamtamkia mtu jambo likawa, haijalishi ni jambo jema au baya.


Kikwazo kikuuu cha kuwakwamisha watu wa MUNGU ni kinywa. (Mithali 18:20-21 ''Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake).


-Kuna mamlaka katika kinywa chako mtumishi wa MUNGU.


-Kuna mamlaka katika kinywa chako wewe uliyempa BWANA YESU maisha yako.

Uwe makni sana na hakikisha kinywa chako kina mema na sio mabaya.


-Kama watumishi wa KRISTO, tukitamka mabaya tujue tunamrudisha YESU KRISTO msalabani.


Haijalishi haya unayatamka kanisani au nyumbani, njiani au kazini.

-Hakuna haja ya kuwa watakatifu kanisani tu, bali tuwe watakatifu na nyumbani pia.


‘’Kinywa changu lazima kitamke mema kwa watu wa MUNGU’’


-Ukikiri uzima utapokea uzima na ukikiri mauti utapokea mauti.

Kiri uzima siku zote za maisha yako.


-Chunga sana mamlaka iliyo katika ulimi wako.

MUNGU amekuwa na mawazo mazuri sana juu yetu, lakini sisi siku zote tunakiri ubaya tu.(Mithali 29:11)

MUNGU hapa anatutamkia mazuri , kwanini sisi kujitamkia mabaya?

‘’MUNGU ana makusudi ya kunibariki’’

Tamka baraka ndugu.



Inawezekana unakabiliwa na mambo magumu katika maisha, lakini kiri ushindi ukisema ‘’sasa naenda kushinda’’ kiri ushindi ukisema sasa naenda kuishi maisha ya ushindi kwa jina la YESU KRISTO.

-Ishi kwa kutamka mazuri tu.

Lazima uishi ndani ya YESU na ukiri ushindi  ukiwa ndani ya YESU.


-Siku zote jifunze kukiri kushinda.

-Enenda kwa imani huku ukikiri ushindi siku zote.

Omba kwa imani na wewe unayeombewa pokea kwa imani.

Imani sio kuona bali imani ni kutarajia na baadae kitu hicho kinakuwa.

''Mathayo 12:36-37-Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.''


-Lazima nitamke vizuri ili hesabu yangu iwe nzuri siku ya mwisho..


-Ndugu yangu linda sana maneno ya kinywa chako maana kila unavyotamkia wengine ndivyo hivyo itakavyokuwa na kwako, pia utatoa hesabu  siku ya mwisho.


Kama maneno ya Daktari yanaweza kumlegeza mgonjwa vipi maneno ya mtu wa MUNGU? Ni zaidi kuliko ya daktari.



-Jifunze kutamka mema tu kwa watu na kwa nafsi yako pia.

''Yakobo 3:9-12-Kwa huo(ulimi) twamhimidi MUNGU Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa MUNGU. Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu.''

Uwe makini sana na kila neno unalotamka au unalotamkia watu.
 

MUNGU akubariki sana na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.


                 MUNGU akubariki sana .

                  Ni mimi ndugu yako

                  Peter M Mabula

         Maisha ya Ushindi Ministry.

                   0714252292

Comments