Kwa mujibu wa afisa polisi wa mji wa Likoni Robert Mureithi amesema mtu
huyo akiwa na bunduki alifyatua risasi ovyo kanisani humo kisha
kukimbia, ambapo majeruhi wamekimbizwa hospitalini kwa matibabu ingawa
haijaelezwa wamejeruhiwa kiasi gani. Mpaka sasa haijajulikana
waliyehusika na tukio hilo ingawa kutokana na mashambulio ya mfululizo,
kuna uwezekano wa kundi la Alshabaab kuhusika na shambulio hilo.
Ingawa pia katika mji wa Mombasa kumekuwa na tabia ya waumini wa dini ya
kiislamu wenye imani kali kutotaka wakristo wawepo katika mji huo ikiwa
pamoja na mji wa Mombasa kujiondoa kwenye jamhuri ya Kenya.Kwa mujibu
wa kamanda Mureithi amesema mpaka sasa usalama umeimarishwa katika eneo
hilo na jeshi hilo limeanza uchunguzi kubaini waliohusika na shambulio
hilo.
Ni hivi majuzi polisi mjini Mombasa waliwakamata watu wawili wakiwa
ndani ya gari na mabomu waliyoyatengeneza ndani ya gari hilo ikielezwa
kwamba mabomu hayo yalikuwa na uwezo wa kuharibu majengo makubwa. Tayari
tahadhari imetolewa nchini humo kuhusiana na matukio hayo ambayo
yanaweza kusababisha maafa makubwa nchini humo, hivyo watu wametakiwa
kuwa waangalifu.
SAMAHANI PICHA ZIFUATAZO NI MBAYA
![]() |
Damu zikiwa zimetapakaa kanisani. |
![]() | |||
Mmoja wa majeruhi akipata matibabu hospitalini © standarddigital news Chanzo:Gospel kitaa |
Comments