MCHAWI AKAMATWA KANISANI

Angalia picha za mtu aliyejitambulisha kwa jina la Shabani Hamisi alikuwa akijihusisha na vitendo vya kishirikina, akiwa chini ya wanamaombi wa kanisa la Ufufuo na Uzima Arusha mara baada ya mtu huyo kukamatwa usiku wa kuamkia leo wakati wa maombi kanisani hapo ambapo ametoa maelezo mbalimbali namna alivyokuwa akishiriki katika vitendo hivyo vya kishirikina.
Shabani akiwa na vitenda kazi vyake akiwa eneo la kanisa.
Akiwa amevua shati huku akiwa anaombewa.
Vitenda kazi vyake vikiwa vimemwagwa chini.


Kazi kwelikweli.
Alikosea njia meeen, akakutana na Yesu meen. Picha kwa hisani ya Ufufuo Crew.
Katika hali isiyo ya kawaida mtu huyu ajulikanaye kwa jina la Shabani Hamis amenaswa akiwa anafanya uchawi katika kanisa la Ufufuo na Uzima Arusha.

Matukio ya kunaswa wachawi yamekuwa mengi kanisani hapo kutokana na uweza wa Mungu unaojidhihirisha kupitia Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo, Frank Andrew.

Pamoja, na kukutwa bila nguo mtu huyo aliyekuwa amebeba vifaa ambavyo kwa mujibu wa maelezo yake, huvitumia kuwanga na kupaa ni pamoja na tunguli na kikapo cha mkoba wa uchawi. Tukio hilo la aina yake limetokea Usiku wa saa sita, wakati mkesha wa maombi ukiendelea kanisani hapo.

Baada ya maombi makali ya kuharibu uchawi katika anga la Arusha, ikafuatiwa na tukio hilo. Mungu ni mkuuu maana hapana uchawi wala Uganga juu ya watu wa Mungu.

Information Ministry - Arusha

Comments