MTUME PETER NYAGA AWSHUKURU WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KWA KUFANYA NAO KAZI YA BWANA

Mungu wetu ni Mungu wa kuinuliwa na kusifiwa na kila mtu. Mungu wetu amekuwa akifanya matendo makuu pkwa kupitia huduma ya RGC Miracle Center chini ya Mtume Peter Nyaga. Tumeona watu wengi wakiokolewa katika mikutano mbalimbali inayofanywa na mtumishi wake na mtiwa mafuta Mtume Peter Nyaga. Mungu amekuwa akisikia maombi ya mtumisjhi wake na kuwaponywa wagonjwa na wenye shida mbalimbali, mapepo yamekuwa yakiwatoka walio wengi na kuwaacha wakiwa huru. Mungu ameleta kicheko na furaha katika familia nyingi kwa kupitia mtumishi wake Mtume Peter Nyaga. Kazi ya Mungu inaonekana machoni mwa walio wengi kwa njia ya ishara na miujiza.
Mtume Peter Nyaga wa kanisa la RGC Tabata Chang'ombe

Kanisa la RGC Tabata Chang'ombe limekuwa bega kwa bega na waimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania kwa kazi ya Bwana. Waimbaji hawa wanatoka katika makanisa mbalimbali lakini wameamua kuungana na Mtume Peter Nyaga kufanya kazi ya Bwana. Hakika huduma yao ya uimbaji imefanyika baraka katika mikutano na semina zinazofanywa na kanisa hili. Mungu azidi kuwalinda waimbaji hawa na kuwapa nyimbo zingine nyingi zenye kugusa nafsi za watu na kuwaokoa.

Tuone baadhi ya waimbaji hawa wakifanya kazi katika moja ya mkutano uliofanywa na kanisa la RGC Tabata Chang'ombe

Kulia ni Neema Gasper
Christina Matai akimtumikia Mungu siku hiyo
Christina Matai
kulia ni Neema Gasper akiwa akifuatiwa na Kenyata

 Tumaini Njole
  Tumaini Njole
Kenyatta

                                    Atosha Kissava


                                   chanzo: Neema Gasper blog

Comments