BWANA YESU asifiwe.
leo tunaangalia mwanzo au chanzo cha wimbo maarufu sana wa tenzi za Rohoni ambao hutumika makanisa yote ya Kikristo. yaani ''NI SALAMA MOYONI MWANGU'' au kwa jina lingine ''NIONAPO AMANI KAMA SHWARI''
Horatio Gates Spafford na Anna Spafford
Katika miaka ya 1860 Horatio aliishi na mke wake
 Anna Chicago,Marekani. Spafford alikuwa
 mwanasheria mkubwa aliyewekeza zaidi kwenye 
majengo (real estates). Maisha yalianza kubadilika
 mwaka 1870 ambapo mtoto wao pekee wa kiume
 alifariki kwa ugonjwa wa nimonia, Mda mfupi baadae
 janga la moto mkubwa wa Chicago uliteketeza 
sehemu kubwa sana ya mali zake.
Wakiwa na matumaini ya kupunguza maumivu
 waliyopata kutokana na matatizo yote,
Mwaka 1873 Spafford na mkewe walikubaliana
 kwenda Uingereza ambapo rafiki yake alikuwa ana
 hubiri injili.
Katika maandalizi ya mwisho kazi zilimbana Horatio, 
Akawaambia mke wake na watoto wake wakike 
wanne watangulie akiahidi kuwafuata haraka.
Ndipo jambo lisiloweza kufikirika likatokea, Boti 
aliyopanda mke wake na watoto wake ikapata ajali 
na watoto wake wote wanne walizama na kupoteza
 maisha, Mke wake pekee alipona nae baada ya
 kufika ufukweni akamuandikia note spaffors ikisema 
"Saved Alone, What shall I do?" yaani "Nimeokolewa
 peke yangu, Nitafanya nini?"
Horatio akiwa njiani kwenda kumfariji mke wake,
 akipita eneo ambalo watoto wake walizama na
 kupoteza maisha ndipo aliandika mashairi ya wimbo
 uliopata umaarufu sana mpaka miaka hii,
Wimbo unaitwa "it is well with my soul" / "Salama
 rohoni mwangu"
Haya hapa mashairi yake kwa kiswahili na kingeleza pia.
1.Nionapo amani kama shwari, Ama nionapo shida; Kwa mambo yote umenijulisha, Ni salama rohoni mwangu.
Salama rohoni, Ni salama rohoni mwangu.
2.Ingawa shetani atanitesa, Nitajipa moyo kwani Kristo ameona unyonge wangu, Amekufa kwa roho yangu.
3.Dhambi zangu zote, wala si nusu, Zimewekwa msalabani; Wala sichukui laana yake, Ni salama rohoni mwangu.
4.Ee Bwana himiza siku ya kuja, Panda itakapolia; Utakaposhuka sitaogopa Ni salama rohoni mwangu.
Wimbo Na. 23
NI SALAMA ROHONI MWANGU1.Nionapo amani kama shwari, Ama nionapo shida; Kwa mambo yote umenijulisha, Ni salama rohoni mwangu.
Salama rohoni, Ni salama rohoni mwangu.
2.Ingawa shetani atanitesa, Nitajipa moyo kwani Kristo ameona unyonge wangu, Amekufa kwa roho yangu.
3.Dhambi zangu zote, wala si nusu, Zimewekwa msalabani; Wala sichukui laana yake, Ni salama rohoni mwangu.
4.Ee Bwana himiza siku ya kuja, Panda itakapolia; Utakaposhuka sitaogopa Ni salama rohoni mwangu.
When peace, like a river, attendeth my way,
When sorrows like sea billows roll;
Whatever my lot, Thou hast taught me to say,
It is well, it is well with my soul.
(Refrain:) It is well (it is well),
with my soul (with my soul),
It is well, it is well with my soul.
Though Satan should buffet, though trials should
 come,
Let this blest assurance control,
That Christ hath regarded my helpless estate,
And hath shed His own blood for my soul.
(Refrain)
My sin, oh the bliss of this glorious thought!
My sin, not in part but the whole,
Is nailed to His cross, and I bear it no more,
Praise the Lord, praise the Lord, O my soul!
(Refrain)
For me, be it Christ, be it Christ hence to live:
If Jordan above me shall roll,
No pain shall be mine, for in death as in life
Thou wilt whisper Thy peace to my soul.
(Refrain)
And Lord haste the day, when my faith shall be sight,
The clouds be rolled back as a scroll;
The trump shall resound, and the Lord shall descend,
Even so, it is well with my soul.
(Refrain)
Baadae Anna alibarikiwa na watoto watatu, Mmoja
 wa kiume ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka
 minne, na wakike wawili. Na baada ya mda walienda
 kuishi Israel na familia yake wakaanzisha kundi la
 kusaidia masikini huko Israel. 
Binafsi Siku ya leo wimbo huu umekua ukijirudia
 ndani yangu kila ninapotafakari matendo makuu
 ambayo MUNGU amenifanyia hasa kwa kipindi hiki
 ambacho nimezungukwa na mambo mengi, siwezi
 kuwaza lolote MUNGU ni mweza wa yote.
angalia video za wimbo huo kwa kiswahili ulioimbwa na waimbaji hawa, katika staili tofauti. 


Comments