NI SALAMA ROHONI MWANGU.


BWANA YESU asifiwe.
leo tunaangalia mwanzo au chanzo cha wimbo maarufu sana wa tenzi za Rohoni ambao hutumika makanisa yote ya Kikristo. yaani ''NI SALAMA MOYONI MWANGU'' au kwa jina lingine ''NIONAPO AMANI KAMA SHWARI''



Horatio Gates Spafford na Anna Spafford



Katika miaka ya 1860 Horatio aliishi na mke wake



 Anna Chicago,Marekani. Spafford alikuwa



 mwanasheria mkubwa aliyewekeza zaidi kwenye 



majengo (real estates). Maisha yalianza kubadilika



 mwaka 1870 ambapo mtoto wao pekee wa kiume



 alifariki kwa ugonjwa wa nimonia, Mda mfupi baadae



 janga la moto mkubwa wa Chicago uliteketeza 



sehemu kubwa sana ya mali zake.



Wakiwa na matumaini ya kupunguza maumivu



 waliyopata kutokana na matatizo yote,





Mwaka 1873 Spafford na mkewe walikubaliana



 kwenda Uingereza ambapo rafiki yake alikuwa ana



 hubiri injili.



Katika maandalizi ya mwisho kazi zilimbana Horatio, 



Akawaambia mke wake na watoto wake wakike 



wanne watangulie akiahidi kuwafuata haraka.



Ndipo jambo lisiloweza kufikirika likatokea, Boti 



aliyopanda mke wake na watoto wake ikapata ajali 



na watoto wake wote wanne walizama na kupoteza



 maisha, Mke wake pekee alipona nae baada ya



 kufika ufukweni akamuandikia note spaffors ikisema 



"Saved Alone, What shall I do?" yaani "Nimeokolewa



 peke yangu, Nitafanya nini?"






Horatio akiwa njiani kwenda kumfariji mke wake,



 akipita eneo ambalo watoto wake walizama na



 kupoteza maisha ndipo aliandika mashairi ya wimbo



 uliopata umaarufu sana mpaka miaka hii,



Wimbo unaitwa "it is well with my soul" / "Salama



 rohoni mwangu"



Haya hapa mashairi yake kwa kiswahili na kingeleza pia.


Wimbo Na. 23

NI SALAMA ROHONI MWANGU
1.Nionapo amani kama shwari, Ama nionapo shida; Kwa mambo yote umenijulisha, Ni salama rohoni mwangu.
Salama rohoni, Ni salama rohoni mwangu.
2.Ingawa shetani atanitesa, Nitajipa moyo kwani Kristo ameona unyonge wangu, Amekufa kwa roho yangu.
3.Dhambi zangu zote, wala si nusu, Zimewekwa msalabani; Wala sichukui laana yake, Ni salama rohoni mwangu.
4.Ee Bwana himiza siku ya kuja, Panda itakapolia; Utakaposhuka sitaogopa Ni salama rohoni mwangu.





When peace, like a river, attendeth my way,



When sorrows like sea billows roll;



Whatever my lot, Thou hast taught me to say,



It is well, it is well with my soul.



(Refrain:) It is well (it is well),



with my soul (with my soul),



It is well, it is well with my soul.



Though Satan should buffet, though trials should



 come,



Let this blest assurance control,



That Christ hath regarded my helpless estate,



And hath shed His own blood for my soul.



(Refrain)



My sin, oh the bliss of this glorious thought!



My sin, not in part but the whole,



Is nailed to His cross, and I bear it no more,



Praise the Lord, praise the Lord, O my soul!



(Refrain)



For me, be it Christ, be it Christ hence to live:



If Jordan above me shall roll,



No pain shall be mine, for in death as in life



Thou wilt whisper Thy peace to my soul.



(Refrain)



And Lord haste the day, when my faith shall be sight,



The clouds be rolled back as a scroll;



The trump shall resound, and the Lord shall descend,



Even so, it is well with my soul.



(Refrain)



Baadae Anna alibarikiwa na watoto watatu, Mmoja



 wa kiume ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka



 minne, na wakike wawili. Na baada ya mda walienda



 kuishi Israel na familia yake wakaanzisha kundi la



 kusaidia masikini huko Israel. 









Binafsi Siku ya leo wimbo huu umekua ukijirudia



 ndani yangu kila ninapotafakari matendo makuu



 ambayo MUNGU amenifanyia hasa kwa kipindi hiki



 ambacho nimezungukwa na mambo mengi, siwezi



 kuwaza lolote MUNGU ni mweza wa yote.

angalia video za wimbo huo kwa kiswahili ulioimbwa na waimbaji hawa, katika staili tofauti.





Comments