Naitwa
prosper kingu kutoka Mtui Mbeli wilaya ya Kiteto mkoani Manyara nimeokoka na
BWANA YESU ni tegemeo langu la uzima wa milele.
Nina mke na
watoto watano, nimeona shuhuda maisha ya ushindi blog na mimi kwa sababu
matukio ya kutisha yameshanitokea, ndio maana nimekutumia na namba yangu ya
simu nimekupa, ili ukweli huu ndugu zangu duniani wauone.
Tumeishi kwa
amani na familia yangu hadi ubaya huu ulipoanza.
Ilianza
vituko nyumbani, siku ya kwanza nijikuta nimelala chini nikajiuliza imekuaje
niwe chini? nikarudi kitandani na baadae nikamsimulia mke wangu ambaye
hakuelewa kilichotokea japo tulikua kitanda kimoja, nikajua ni mzaha tu.
Baada ya
wiki moja vituko vikazidi, hali ya maisha yalikua magumu sana katika kijiji
chetu na siku moja tulilala bila taa kwa
sababu hatukua na pesa ya kununua mafuta ya taa, lakini usiku tukakuta taa
inawaka, imejaa mafuta na kiberiti kipya mezani. tuliogopa sana lakini nilijua itaishia hapo. cha ajabu siku iliyofuata baada ya chakula
cha usiku tuliingia kitandani na mke wangu nilivaa bukta na mke wangu alikua
anataiti tu. usiku wa manane tukajikuta tupo uchi kabisa. na mke wangu
amevishwa shanga kiunoni na moja ya shanga ina hirizi kubwa kama kidole gumba cha
mkono, nikashangaa sana na kuhofu mno tukashauriana
na mke wangu kwenda kufanyiwa maombi
kanisani. Palipokucha zile shanga na hirizi
hazionekani, kutokana na ugumu wa
maisha nilikimbilia kwanza kazini na nilirudi saa 10 jioni, nimechoka sana nikajipumzisha
kwenye kochi na usingizi ukaanza kunichukua. mke wangu akanisistiza kwenda kwa mchungaji kuombewa. Nikaanza kumpigia simu mchungaji, ila sio
mchungaji kwa sababu mchungaji wangu alikua masomoni, ilikua saa 1 usiku.
Mchungaji
akaniambia njoo utanikuta kanisani. nikaondoka.
Kumbe wakati
naenda kanisani nilitekwa njiani bila kujua. Nikizani naenda kanisani kumbe
lah! nikaingia kwenye ofisi niliyodhani ni kanisani na kwa akili yangu ya
kibinadamu na uenyeji wangu pale nilidhani ni kanisani kumbe hata sijui ufahamu
wangu ulikua umechukuliwa maana kilichotokea ni cha ajabu mno. Nilipokaribia
ofisi ile, mbele yangu nikamuona mtu kama mchungaji niliomhitaji, akaniuliza
prosper umekuja? nikamjibu ndio
mchungaji. Nikaingia ndani na mlango ukajifunga pale pale yule niliodhani ni mchungaji akawa binti mzuri
wa kiarabu na mazingira yakabadilika ghafla, pakawa na sofa za nguvu na marashi
yakuvutia. niliogopa sana lakini yule binti alinibembeleza na kutaka niseme
chochote ninachotaka atanipa. nilichukua muda kumjibu. baada kama dakika 5
nikasimama ili nitoke nje lakini mlangoni nikakuta watu wawili wakanizuia
nisitoke, sikua mbishi nikarudi kwenye sofa. yule binti akaanza manjonjo ya
kimapenzi, akavua nguo zote na akanivua nguo zote, tukabaki uchi, akanikalia
mapajani na kunibembeleza niseme ninacho kitaka atanipa. Nililia sana, nikawaza
familia yangu, kanisa, majirani na mambo mengi yanayo nizunguka. ukweli ni
kwamba maisha yangu yalikua duni sana. lakini sikuwaza utajiri wa dunia hii. Niliwaza
maisha ya milele baada kufa. Nilijua huo ndio utakuwa mwisho wangu maana dakika
chache baadae ningekufa na nilijua nipo
kuzimu.
Nilijuta
makosa niliyo yafanya duniani. sikumjibu yule binti kwa muda wa kama dakika 90, baadae
nikapata ujasiri kidogo. Nikamuuliza.
Namtaka YESU akanijibu "hapatikani hapa" nikamwambia "Sihitaji
chochote zaidi ya YESU" Nikaanza kuomba kwa sauti ya chini, nikazidi
kupata ujasiri. nikasimama kuelekea mlangoni sikuona aliyenizuia tena, nikatoka
nje ya lile jengo na kuelekea nisipo pajua. kwa mwendo wa kama masaa mawili ila
nikiwa uchu bila nguo hata moja maana wakati nasimama kuondoka hata nguo zangu
sikuziona. Ndipo nikajua kumbe nipo mwisho wa mji na nyumbani kwangu una mwendo wa nusu saa. lakini nipo uchi
kabisa huo na ni kama saa 8 usiku, mwezi unawaka maana hakukuwa na wingu kabisa
muda ule. Nilijisemea moyoni kwamba, naenda nyumbani nitakayekutana nae njiani
yeye ndiye mchawi, sio mimi na sipiti uchocholoni, nikaanza safari hiyo ya
kwenda nyumbani.
Nilipokaribia
nyumbani nikasikia mke wangu na watoto wanamwomba MUNGU maombi ambayo sio ya
kawaida. Nikasimama nje nikashiriki maombi na familia yangu kwa muda kama wa
dakika 10, nikagonga mlango na kumwambia mke wangu aje na kanga kwa sababu niko
uchi. Mke wangu akazuia watoto wasitoke, akanisitiri kwa mavazi ndipo nikaomba
niwaone wanangu. Ilikuwa ni usiku wa majonzi sana siku hiyo na cha ajabu wakati
wa matukio ya kule kwenye jengo la ajabu, mke wangu alikuwa anatumiwa sms
kutoka namba ya kiarabu na maneno ya kiarabu kujurishwa kinachoendelea akaomba
msaada kwa kijana mmoja mmoja mlokole ambaye walianza kuomba pamoja, lakini
baadae yule kijana aliondoka kurudi nyumbani, lakini alianza tu safari kutoka
kwangu, nyuma yake kulikuwa na watu wakimfuata hadi nyumbani kwake. Alipofika
akamhadithia mke wake kisa cha
kuchelewa, alipokuwa akimsimulia mke wake
wakaanza kusikia wanapita juu ya
nyumba yao wakiongea lugha isiyoeleweka, yalikuwa ni majini maana hawakulala
siku hiyo bali walikesha wakiomba hadi asubuhi
walipojiandaa kwenda kanisani, na walipofika kanisani yule kijana
ilibidi atoe ushuhuda wa mambo yaliyotokea usiku. Kanisa likaomba na yule kijana akaambiwa apige magoti ili
aombewe lakini alishindwa maana miguu
yake ilikuwa inauma sana kama, alianza kuona magoti yake yanachomwa na sindano
ila hakuwaona wachomaji, mambo yalipokuwa magumu aliwaeleza wana maombi tatizo
hilo na hakika ilikuwa ni huzuni kanisani maana kila mmoja alishangaa na
kushtuka sana. Baadae mimi na familia yangu tulifika kanisani lakini kwa sababu
nilikuwa na majonzi sana sikuweza
kushuhudia bali kulia tu maana nilikuwa nalia kama nimefiwa. Lakini kwa maelezo
machache niliyoyatoa kanisa lilichukua mzigo wa kufunga siku 3 bila kula usiku
na mchana. Baada ya maombi hayo kumalizika nilikuwa bado niko kanisani alikuja
mwanangu wa darasa la 7 Irene Prosper kutoa taarifa kwamba amezikuta nguo zangu chini ya kitanda alipokuwa
akifanya usafi. Ndipo kanisa likazidi kuomba
kwa bidii baada ya kuona dalili
za ushindi. Siku ya jumamosi ilikuwa ni siku ya kumpokea mchungaji wetu akitoka
masomoni. Mchungaji Denis Majelanga alipokuta kanisa lina pigo alitangaza
maombi ya siku 7 ya kupokezana. Ndipo nilipoona ushindi wa ajabu sana kutoka
kwa MUNGU, Maana katikati ya mataifa na kijiji chote cha matui kikajua kweli
kwamba yupo MUNGU katika waliookoka.
Mama
mmoja aliyekuwa na ukaribu sana na mke
wangu alipoteza line yake ya simu , ikaokotwa
na fundi mmoja wa nguo,
alipojaribu kuiweka kwenye simu yake
aligundua kuwa mwenye hiyo line ana mawasiliano na watu wasioishi katika hii dunia, na watu hao
wasioishi katika hii dunia walikuwa wakimtaka yule mama aliyepoteza line kwamba
anakikishe ananiteka na kufanya mapenzi
na mimi ili nianguke katika wokovu. Kwenye hiyo line kulikuwa na meseji alizotumiwa ili afanye mazingaombwe ya kuhakikisha zoezi la kuninasa, na mipango yote ilifanyika hadi nafika kwa yule binti wa
kiarabu(kuzimu) ni yeye aliifanya. Huyo
mama baada ya kugundua amepoteza hiyo line
na imeokotwa aliondoka hadi kwa mchungaji Denis kumuomba / kutuomba
msamaha juu ya yote aliyoyatenda na alikiri kwamba yote yaliyotupata ni
yeye ndio mhusika mkuu. Mchungaji
alikuja nyumbani na huyo mama, alipotoa
maelezo yake! Jamani nilikosa pozi na
kuwaza tu kwamba kweli ‘’dunia ina mambo.’’ Kumbe kuna watu wanaendeshwa na rimoti za
kuzimu. Baada ya maelezo ya mchungaji, nilimsamehe yule mama ila nilimsihi
aokoke, na siku hiyo akaongozwa sala ya toba upya. Na kuokoka upya licha ya
kuwa mshirika wa miaka mingi ila kumbe hakuwa na ushirika na BWANA wetu YESU
KRISTO ila alikuwa na ushirika na majini.
MUNGU
awabariki sana na akubariki sana
Mtumishi wa Maisha ya ushindi kwa kuuweka ili watu waone yaliyonikuta.
Namba yangu
ya simu ni 0717452412 kwa yeyote
atakayetaka nimusimulie live ,maana nimefupisha tu kwa baadhi ya maeneo
ila uweke hivyo hivyo ila kuhusu picha siku nikipata mtu anayetumia fecebook
nitakutumia ili uweke na picha.
Amen amen amen
Kutoka Maisha ya ushindi blog
Ubarikiwe sana
mtumishi na asante kwa kushuhudia ili tumtukuze MUNGU pamoja, Biblia inasema
kwamba ‘’Aliye na Mwana wa MUNGU, Hakosi ushuhuda’’
Tena
tunamshinda shetani kwa damu ya Mwanakondoo YESU KRISTO na kwa neno la
ushuhuda(Ufunuo 12:11).
Songa mbele
na tuko pamoja na pia kama kuna mtu unayemfahamu anaushuhuda wa kweli nijurishe
ili tuendelee kumwaibisha shetani.
KUSHUHUDIA
NI KUMWAIBISHA shetani.
UBARIKIWE
SANA
Comments