TUKISHINDA YA DUNIA KUNA TAJI YA UZIMA.





BWANA YESU asifiwe.


Karibu tena tujifunze jambo muhimu kuliko yote wanalotegemea wanadamu wote yaani TAJI YA UZIMA, ambapo taji hiyo wanaipata walioshinda ya dunia na kuingia UZIMA WA MILELE kupitia YESU KRISTO.


1 Korintho 9:25-Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee TAJI ISIYOHARIBIKA


-Heri mtu yule astahimiliye majaribu majaribu ya dunia maana akishinda atapokea TAJI YA UZIMA.

Yohana 3:16 inatuonyesha mwanzo wa taji ya uzima ambapo MUNGU anamtoa BWANA YESU kwa ajili ya kila mwanadamu ambaye atapenda kuwa UZIMANI.( Kwa maana jinsi hii MUNGU aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.)


-Uzima ni kitu cha kwanza.


-Kila mtu anahitaji uzima.


-Wanadamu wote walikuwa wamepungukiwa na utukufu wa MUNGU, lakini kwa mmoja tu(YESU KRISTO) tunapata uzima wa milele.


Yakobo 1:12. -Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea TAJI YA UZIMA, BWANA aliyowaahidia wampendao.


Tunatakiwa tupate uzima wa milele, ila majaribu yapo lakini atakayestahimili mpaka mwisho wa maisha yake ataipata taji ya UZIMA WA MILELE.


-Duniani ni njia ya tu ya kwenda katika makazi ya milele.

Makazi ya milele yapo ya aina mbili.


               1.  Makazi ya uzima wa milele.

               2.  Makazi ya mateso milele.


Najua kila mtu anahitaji UZIMA WA MILELE. Na uzima wa milele unapatikana katika KRISTO YESU pekee(Yohana 14:6,  NA PIA Matendo 4:12- inayosema ‘’Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.’’).


Uzima wa milele ni muhimu sana, na ni hakika kila mtu anamhitaji BWANA YESU ili apone kutoka kwenye mikono ya shetani.


Asante sana BWANA YESU kwa uzima wa milele.


Ufunuo 2:10.- Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa TAJI YA UZIMA.


-Wengi sana wanaompenda MUNGU, hupenda baraka zake tu, lakini wakipata majaribu kidogo hugeuka na kuonyesha kabisa kwamba hawampendi MUNGU.


-Tunaweza kuwa na furaha wakati wa dhiki, kama tu ROHO MTAKATIFU  yuko ndani yetu.


-Taji ya uzima tunaipata katika KRISTO tu.


BWANA YESU anasema katika Ufunuo 22:12-13’’Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.


TUMPELELEZE NANI HABARI ZA MBINGUNI?

Tumpeleleze nani habari za mbinguni?

Tumpeleleze nani habari za uzima?

Tumpeleleze nani habari za uponyaji?

Tumpeleleze nani habari za mafanikio?

Tumpeleleze nani mambo ya mbinguni?

YESU NDIYE WA KUMPELELEZAAAAAAAAAAAAA.

YESU ndiye wa kumpeleleza maana yeye anao UZIMA.


Songa mbele na BWANA YESU ndugu.

Hakuna uzima kwingine kokote ila kwa YESU KRISTO pekee.


Asante BWANA YESU kwa uzima.

Asante YESU unayeokoa.

Asante YESU utupaye TAJI YA UZIMA.

Zaburi 16:11’’Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele.’’
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                     MUNGU akubariki sana .
                      Ni mimi ndugu yako
                       Peter M Mabula
                 Maisha ya Ushindi Ministry.
                           0714252292

                    mabula1986@gmail.com
                 MUNGU akubariki sana
uliyesoma somo hili.
                      MUNGU Akubariki.

                

Comments