Ukiwa na uraia wa mbinguni utalindwa na serikali ya mbinguni.

Ukiwa Mmarekani, Serikali Ya Marekani Itafanya Chochote Kukulinda Ama Kuhakikisha Usalama Wako... Ikitokea Adui Akamgusa Mmarekani Au Kumdhuru, Serikali Ya Marekani Huwa Hailichukulii Kwa Urahisi Jambo Kama Hilo... 

 Sipati Picha Ukiwa Mkristo, Raia Wa Serikali Ya Mbinguni; MUNGU, Rais Wa Serikali Ya Mbinguni Anakuwa Ukuta Wa Moto Kukuzunguka Na Utukufu Ndani Yako, Anakuzunguka Kama Milima Iizungukavyo Yerusalemu, Anakuwa Adui Wa Adui Zako, Anakuwa Ngome, Kimbilio, Msaada Na Nguvu Zako... 

Huhitaji GPS Kwa Ajili Ya Kuku-locate; Amekuchora Kwenye Kiganja Chake, Kuta Zako Zi Mbele Zake Daima, Jicho Lake Linazungukazunguka Duniani Ili Ajionyeshe Mwenye Nguvu Kwa Ajili Yako, Anakupa Fursa Ya Kuwa Mrithi Pamoja Na KRISTO, 

Anakuhakikishia Kukupatia Hazina Za Gizani Na Kukupa Kabila Za Watu Kwa Ajili Ya Maisha Yako, Anakuhakikishia Kustawi Mjini Na Mashambani, Anakufungulia Mlango Wa Mafanikio Kwa Kila Ulifanyalo Sawa Na Mti Uliopandwa Kando Ya Vijito Vya Maji, 

Anakupa Uhakika Wa Kuwa Juu Tu Na Wala Sio Chini... Anakupa Access Ya Kufanya Mawasiliano Moja Kwa Moja Na Yeye Kupitia MTANDAO Huitwa JINA LA YESU, Ambao Unakuhakikishia Kushughulikiwa Kwa Hitaji Lako! Haiishii Hapo, Anakuwekea Majeshi Ya Malaika Ili Wakulinde Na Kukuokoa, Na Anawaagiza Wakuongoze Hadi Mahali Alipokutengenezea, Wanakuwa Pamoja Nawe Muda Wote Maana Hao Ni Watumishi Wako Wewe Utakayeurithi Uzima Wa Milele! 

Kubwa Zaidi, Unao UZIMA WA MILELE; Aina Ya Uzima Alionao Mungu, Unaokupa Tiketi Ya Kufanya Vitu Kwa Kiwango Cha Mungu...Kwa Leo Inatosha Mwanafunzi Wangu Mwema! AM PROUD TO BE A CHRISTIAN; THE CITIZEN OF HEAVEN AND THE AMBASSADOR OF CHRIST ON EARTH"

Comments