Upendo kilahiro afanya Live DVD Recording ya Praise and worship ndani ya VCCT jijini Dar es Salaam


Mwanamuzi maarufu wa nyimbo za injili kutoka jijini Dar es Salaam Upendo Kilahiro pamoja na Mume wake Amon Kilahiro jumapili hii wamewaongoza maelfu ya Wakazi wa Jiji la Dar-es-Salaam katika Ibada ya Kumwabudu Mungu jioni ya Leo ambayo imefanyika live na kurekodiwa ambapo baadae itapatikana katika mfumo wa DVD .
Addo November akienda Sawa na Upendo Kilahiro
Katika Live Recording hiyo mwanamuziki huyo amesindikizwsa bega kwa bega na wanamuziki mbalimbali machachari wa muziki wa injili toka Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na Addo November, Glory Kilahiro na The Voice.

Mamia ya wakazi wa jiji la Dar-es-Salaam waliojitokeza katika Live Recording hiyo walionekana wakimwabudu Mungu Muda wote wa Ibada hiyo ya kusifu na Kuabudu.


picha za tukio hilo ni kama zinavyoonekana hapa chini.

Ma Mc wa Event Pastor Mwita pamoja na Double G, Godwin Gondwe wakienda sawa
  Mpiga Saxerphone Maarufu Mise Anaeli akienda sawa katika Live Recording ya Upendo Kilahiro
 
  Mise Anaeli akikamua tarumbeta
  Mise akienda sawa na Upendi Kilahiro

Music Arranger Samuel Yona akiwa kikazi zaidi
  Fredy Msungu akiwa anaenda Sambamba na Addo na Upendo Kilahiro
  Wadau wa Muziki wa Injili Wakiwa ndani ya Ukumbi
  The Voice Wakiimba Acapella Upendo Kilahiro

                                                               Credits:Samsasali blog

Comments