BREAKING NEWS: MKURUGENZI WA WANAWAKE WA INJILI EAGT AFARIKI DUNIA

Ailyekuwa mkurugenzi wa WWI Taifa, EAGT - Mama Benja, enzi za uhai wake.
Taarifa za kusikitisha ambazo zimetufikia hivi punde ni kwamba mkurugenzi taifa wa wanawake wa injili wa kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania anayefahamika kwa jina la Mama Benja, amefariki dunia.

Kwa mujibu wa familia, hadi mauti yanamkuta Mama Benja, presha ilikuwa chini kiasi cha kulazwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mbeya. Taarifa zaidi zinaeleza kuwa maazishi yatafanyika siku ya Jumanne mkoani Mbeya.

Miaka ya 1974 huko Bugando mjini Mwanza ndipo historia ya Mama huyu imetambuliwa kuanzia, ambapo alikuwa mmoja wa viongozi wa WWK enzi hizo kanisa la Bugando (alikoanzia marehemu Askofu Moses Kulola) likiwa chini ya TAG, wakati huo pia mume wake akiwa mzee wa kanisa. Miaka 6 iliyopita alikuwa makamu wa WWI EAGT na hatimaye 2011 kuwa Mkurugenzi kamili.

Licha ya kuwa muinjilisti wa muda mrefu zaidi, shujaa huyu wa injili kwa zaidi ya miaka 30 amekuwa pia kiongozi wa wamama kwa kipindi kirefu akishika  nyadhifa mbalimbali.

Tutaendelea kukufahamisha zaidi kwa kadri taarifa zitakavyokuwa zikitufikia, kaa na GK. BWANA ametoa, na BWANA ametwaa, jina la BWANA lihimidiwe.

Marehemu mama Benja kwenye maazishi ya aliyekuwa makamu mkurugenzi wa Wanawake wa Injili taifa, Mama Nyanda.Chanzo:Gospel Kitaa     

Comments