Happy Birthday TANZANIA. MUNGU akulinde taifa letu.

 Leo tarehe 26 April muungano wa Tanganyika na Zanzibar umetimiza miaka 50. Tunamshukuru MUNGU kwa hatua hii njema . Maombi yangu amani iendelee siku zote na Bunge la katiba wafanye maamuzi mazuri ya kuwapendeza watanzania wote.
Hongera Tanzania.
Hongera nchi yangu.
MUNGU ibariki Tanzania.
MUNGU wabariki watanzania wote.
Katika jina la YESU KRISTO amen.
 
 
 
 
Waasisi wa Muungano wa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (kushoto) na Hayati,  Abeid Aman Karume (kulia waliokaa) wakisaini nyaraka za Muungano mwaka 1964.
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akichanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, huku akishuhudiwa na Rais wa Zanzibar, Abeid Aman Karume, (wa tatu kushoto) na Mhe. Rashind Mfaume Kawawa (wa kwanza kulia) wakati wa sherehe za kwanza za Muungano zilizofanyika Tarehe 26 Aprili, 1964.
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (kushoto) na  Sheikh Abeid Amani Karume (kulia) wakibadilishana Hati za Muungano wa Tanganyika na  Zanzibar Aprili, 1964.
Waasisi wa Muungano, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (kushoto) na Hayati Abeid Aman Karume.

Comments