HATIMAYE JOHN SHABANI AHITIMU MASOMO YAKE KWA NGAZI YA DEGREE

John akiwa na uso wa furaha baada ya kumaliza masomo yake kwangazi ya degree (Bachelor of arts in Biblical Studies)


 Mmoja wa wakurugenzi wa chuo hicho, Dr. Lee, akiwapiga wanafunzi msasa wiki moja kabla ya mahafali



 John Shabani na mwandishi wa habari, George Kabula


 Elimu haina umri, huyu hapa ni bibi wa miaka 80 akifurahia kumaliza masomo yake
Mary B. Nyerere
Baadhi ya wanafunzi waliohitimu masomo yao kwa ngazi ya diploma


Imekuwa siku ya furaha na shangwe kwa wanafunzi, ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria katika mahafali ya pili ya chuo cha kimataifa cha Biblia (International School of ministry – ISOM), tawi la Tanzania. Kwa mara ya pili sasa, lakini pia ni mara ya kwanza kwa ngazi ya degree au BA (Bachelor of arts in Bible knowledge)

Chuo cha ISOM kikishirikiana na chuo kikuu cha uongozi (Christian Leadership University) vyenye makao makuu huko Marekani, kwa mara ya kwanza Tanzania, wametoa vyeti kwa ngazi ya shahada na stashahada (Diploma and BA).

John Shabani ni kati ya wanafunzi waliotunukiwa cheti kwa ngazi ya degree. Kabla ya kuhitimu, chuo kilipata bahati ya kutembelewa na mmoja wa viongozi wa ISOM kutoka Marekani, Dr. Lee. Kiongozi huyo aliwapiga msasa wanafunzi kwa muda wa siku tatu.

Usajili wa wanafunzi wapya unaendelea.

Comments