Shalom watu
wa MUNGU.
BWANA YESU
asifiwe.
Mimi ni
mzima na nakukaribisha tujifunze somo
hili ambalo MUNGU amenipa kwa ajili yako
, na yangu na ya wengine wote watakaosoma miaka yote.
''Mithali
18:10- Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia akawa salama.''
-Mambo
mawili(2) makubwa yanapatikana kwenye mstari wa Biblia hapo juu.
1: JINA LA
BWANA NI NGOME IMARA.
2: MWENYE
HAKI HUIKIMBILIA AKAWA SALAMA.
Umuhimu wa
mambo haya mawili unategemeana yaana mwanadamu anahitaji kitu kwa BWANA na
BWANA anaangalia sifa za mwanadamu huyo mhitaji, kama anastahili kupokea au
hastahili.
1: JINA LA
BWANA NI NGOME IMARA.
BWANA hapa
ni MUNGU mwenyezi.
MUNGU
ameiweka ngome imara ndani ya jina la YESU KRISTO.(Wafilipi 2:9-11, Kwa hiyo tena MUNGU alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
ili kwa jina la YESU kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa MUNGU Baba.
).
Kwa hiyo
jina la BWANA YESU ni ngome imara,
BWANA YESU
ndiye ambaye jina lake pekee tunaweza kuomba kwalo na kupokea.
Jina la YESU
KRISTO ndilo jina kuu kupita majina yote, na jina hili BWANA YESU alipewa na
MUNGU Baba.
Hata ujio
wake hapa duniani, malaika wa MUNGU alisema yafuatayo kwa Yusufu mchumba wa
Mariamu. ‘’Mathayo 1:21-Naye(Mariam) atazaa mwana, nawe utamwita jina lake
YESU, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.’’
-Hivyo jina
la YESU KRISTO ni ngome imara, na pale linapotajwa uzima unaingia. Nimewahi
kuona kwa macho yangu jina la YESU KRISTO likitajwa na uzima kutokea. Dda mmoja
alipona ukimwi mbele ya macho yangu kule Zanzibar maana aliombewa na kwenda
kupima na kuleta majibu kutoka hospital 3 alizokua amenda kupima, kote huko
walimwambia amepona, UTUKUFU KWA BWANA YESU. Watu wengi wamepona kifua kikuu,
Malaria, uvimbe tumboni, kuharibika sehemu za siri na kila ugonjwa na kila
udhaifu.
HAKIKA JINA
LA BWANA YESU NI NGOME IMARA.
NGOME ni
ulinzi uliozunguka pande zote, kama askari wataweka ngome sehemu fulani ina
maana kila upande wa eneo kutakuwa na ulinzi, tena masaa yote, ni ngumu sana
kuingia kwenye ngome kama hii. Lakini jina la BWANA YESU ni zaidi ya hizo ngome
za kibinadamu. Zaburi 27:1b inasema ‘’BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?’’
Ndugu
kimbilia kwenye ngome hii leo, kuingia kwenye ngome hii ni bure kabisa.
2: MWENYE
HAKI HUIKIMBILIA AKAWA SALAMA.
Jambo la
pili katika andiko tuliloanza nalo ni MWENYE HAKI AKIKIMBILIA ANAKAA SALAMA.
Mwenye haki
ni mtu gani?
Na kwa nini sio kila mtu akikimbilia ngome hii anakua salama?
Na kwa nini sio kila mtu akikimbilia ngome hii anakua salama?
Je haki hii inatafutwaje?
Je haki hii
hudumu kwa muda gani?
Je tunalipia
pesa kiasi gani kuipata hii haki muhimu maishani?
Yawezekana
unajiuliza maswali kama hayo hapo juu na hujapata majibu.
Ndugu haki
hii ya kuiendea ngome hii na ukawa salama unaipa kwa kumpokea BWANA YESU.
(Yohana 1:12-13Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake;
waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU.
).
Jambo kuu
kwa kila mwanadamu ni kumpokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yao.
BWANA
wenyewe anasema kwamba kama tukimkabidhi maisha yeye. Yeye(YESU) na BABA yake
watakuja na kufanya makazi ndani yako yaani kwa maana nyingine watakuja na
kuweka ngome ndani yako.
-Mwenye haki
wa kuiendea ngome hii ni yule aliyemkabidhi BWANA YESU maisha yake.
-Haki hii
inatafutwa kwa wewe kuokoka na kulikulia neno la MUNGU pamoja na wengine
kanisani.
-Haki hii
hudumu siku zote za maisha yako kama tu na wewe utadumu kukaa ngomeni yaani kwa
YESU KRISTO.
-Huhitaji
kulipa pesa ili kuipata haki hii muhimu bali ni wewe tu kumpokea BWANA YESU.
Warumi 10:9 -11 ( Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa
chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua
katika wafu, utaokoka.
Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika.
).
-Baada ya
wewe kuipata haki hii muhimu , kinachofuata ni wewe kuifuata ngome hii imara
kwa maombi na hakika utakaa salama. Yeye MUNGU anasema hivi juu ya mtu
uliyetimiza vigezo hapo juu (Isaya 54:17,Kila
silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka
juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa
watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.
)
Tena BWANA anasema kwamba juu yako mwenye haki ambaye umeamua kukaa ndani ya KRISTO maisha yako yote. Yeremia 1:19 ,(Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema BWANA, ili nikuokoe. )
Tena BWANA anasema kwamba juu yako mwenye haki ambaye umeamua kukaa ndani ya KRISTO maisha yako yote. Yeremia 1:19 ,(Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema BWANA, ili nikuokoe. )
Ndugu zangu
ni furaha sana kuwa ngomeni mwa BWANA YESU, Wacahwi watakuogopa wewe badala ya
wewe kuwaogopa, na BWANA anasema kwamba Yohana 14:14, ( Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.
)
Ndugu zangu
watu wa MUNGU wakati mwingine tunakosea kwa kuwa ngome wa BWANA YESU lakini
tunashindwa kuomba au kukimbilia badala yake tunataka kutumia akili zetu wenyewe
na wengine kwa sababu ya maarifa yao ya kibinadamu wanajaribu kuishi bila
kumtegemea BWANA . ni mbaya sana.
Naomba tuwe
na haki siku zote na siku zote tulikimbilie jina la BWANA YESU ili tukae salama
siku zote.
Unganisha
jina la YESU KRISTO na haki yako uliyopewa na MUNGU ili uombe na kukaa salama ,
omba pia kwa ajili ya ndugu zako, familia yako na taifa lako. Maana wewe ukiwa
ngomeni mwa YESU unauwezo wa kuwasaidia hata ndugu zango maana haki yako
itasikiwa na MUNGU na watakuwa salama wao kwa sababu ya maombi yako.
-Pia
usisahau kwamba shetani naye huweka ngome zake lakini wewe uliye na ngome ya
jina la YESU KRISTO unaweza kuziangusha ngome zote za giza kama walivyofanya
hivyo watumishi wa MUNGU wa zamani ona mfano jinsi Daudi alivyoangusha ngome za
adui 2 Samweli 5:7-10( Lakini Daudi aliipiga NGOME ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi.
..................Naye Daudi akazidi kuwa mkuu; kwa maana BWANA, MUNGU wa majeshi, alikuwa pamoja naye.
) na Daudi kwa
sababu anamjua MUNGU wake anasema katika 2 Samweli 22:2 kwamba ‘’BWANA ndiye
jabali langu na mwokovu wangu, naam,
wangu’’ na katika Mstari wa 33 wa hiyo hiyo 2 Wafalme 22 Daudi anasema ‘’MUNGU ndiye ngome yangu yenye nguvu, Naye
huwaongoza wakamilifu(wenye haki) katika njia yake’’
JINA LA
BWANA YESU HAKIKA NI NGOME IMARA SANA, TUKIMBILIE LEO ILI TUWE SALAMA.
MUNGU
akubariki sana na kama
hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa
mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na
wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU
akubariki sana .
Ni mimi
ndugu yako
Peter M
Mabula
Maisha ya
Ushindi Ministry.
0714252292
Comments