KWANINI IMANI NI MUHIMU SANA KWA MKRISTO?



 
BWANA YESU asifiwe ndugu zangu.


Namshukuru MUNGU wa mbinguni kwa uzima wake kwangu na kwako pia maana uzima aliotupa MUNGU ndio chanzo cha sisi kukutana hapa kupitia neno la MUNGU.


Imani ni muhimu sana kwa kila mkristo kwa sababu mambo yote ya wokovu tunayapokea kwa imani.

-Mambo ya uponyaji tunapokea kwa imani.

-Majibu ya maombi tunapokea kwa imani.


Imani ni kuwa na uhakika wa mambo unayotarajia, ni mambo yasioonekana lakini kwa imani huja na kuonekana.

Waebrania 11:1-( Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.   )



-Ukimwendea MUNGU kwa maombi , au kwa sadaka au kwa chochote, lazima uende kwa imani.


-Hata wokovu wetu tumeupata kwa imani.

Waefeso 2:8-10 (  Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha MUNGU; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika KRISTO YESU, tutende matendo mema, ambayo tokea awali MUNGU aliyatengeneza ili tuenende nayo. )


Imani sio kipofu, imani inaona, imani ina macho; Na mtu wa imani anaona kabisa kwamba anapona kweli.


Sura ya Waebrani 11 inaitwa UKUMBI WA MASHUJAA WA IMANI.


Mwanamke mmoja  alisima katika maombi akitumia Waebrania 11:35a( Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. ), baada ya mme wake kufariki kwa ajali huku huyu mwanamke akiwa mjamzito. Lakini kwa imani katika maombi , aliomba hadi mme wake akafufuka baada ya siku 4 akitumia andiko hilo. Maana baada ya siku 4 za maiti yake kuwa mochwari na hadi kufikia hatua ya kuganda. Siku ya 4 baada ya mwili kuganda kwa sababu ya kukaa mochwari lakini siku ya 4 Waliibeba maiti na kuipeleka kwenye mkutano wa Reinhard Bonke, walipofika kwenye mkutano wahudumu waliogopa kuipeleka maiti mbele ili kuombewa maana mawazo yao yalikuwa je kama asipofufuka itakuwaje?

Yule mama kwa imani kubwa alikuwa akiwasisitiza wampeleke mmewe mbele akaombewe lakini wahudumu waligoma, na kuipeleka nje ya mkutano lakini wakati wa maombezi Nguvu ya MUNGU ilishuka na yule maiti akaijiwa na uhai maana kwanza wakati maombezi yakiendelea  barafu ilianza kutoka katika mwili wa ile maiti na baada ya muda yule maiti alisikika akisema ‘’ faili langu faili langu’’. Kumbe alikuwa mbinguni kwa siku 4 lakini kwa imani mke wake aliomba na kuomba sana akitumia Hiyo Waebrania 11:35a. N hadi sana ni watumishi wa MUNGU; na hii ilikuwa ni Nigeria.


IMANI INANGUVU, IMANI INAONA, IMANI UNAAMINI .


-Ukisimama katika neno la MUNGU kwa maombi ya imani, MUNGU anatenda kupitia neno hilo.


-YESU KRISTO ni yeye yule, jana na leo na milele na yote kwake yanawezekana kwa yule mwenye imani aaminiye.


-Imani ni kuwa na ufahamu na uhakika wa mambo tusiyoyaona.

KATIKA IMANI: Unakuwa na uhakika na MUNGU unayemwendea.


IMANI inajua kwamba MUNGU anaweza yote.

Huwezi kumpendeza MUNGU kama huna Imani.



MUNGU awabariki sana kwa tafakali hiyo.
 na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.



                       MUNGU akubariki sana .

                        Ni mimi ndugu yako

                          Peter M Mabula

                    Maisha ya Ushindi Ministry.

                         0714252292

Comments