MUNGU amtumia mchungaji Gwajina kuwaweka huru wajapani.kutoka mikononi mwa shetani.


NI MUENDELEZO WA ZIARA KUBWA YA KUHUBIRI INJILI  DUNIANI KOTE NA MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA ANAENDELEA KUTUMIWA NA MUNGU BABA WA MBINGUNI KATIKA VIWANGO VYA JUU SANA

Mchungaji Josephat Gwajima ameshafanya mikutano mikubwa ya Injili katika miji mbali mbali nchini Japani, miji hiyo ni Osaka, Nagawa, Hiroshima,na sasa ni Nagoya na bado Yesu Kristo aliyeishinda mauti anaendelea kutenda miujiza ya kupita fahamu za wanadamu nchi humo.

Yafuatayo ni matendo na miujiza mikubwa ambayo Mungu ameyatenda kupitia kwa Mchungaji Josephat Gwajima katika mwezi huu wa April,2014 nchini Japan


Mchungaji wa nchini Japan akimkaribisha Mchungaji Josephat Gwajima katika mkutano uliokuwa na Nguvu za Mungu za kupita kawaida, Jijini Nagoya nchini Japan

Mchungaji Josephat Gwajima akianza kuhubiri na kushoto kwake ni mkalimani ambaye ni mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Tawi la Japan
Baadhi ya wachungaji na washirika wakiwa wanamsikiliza Mchungaji Josephat Gwajima kwa umakini....


Mchungaji Josephat Gwajima akiwa anafundisha mjini Nagoya,Japan


Nchi ya Japani imejaliwa watu wa Mungu wenye kusifu sana...






Ukafika muda ambao Roho Mtakatifu kujidhihirisha kwa nguvu na mamia ya watu waliojazana ukumbini kunena kwa Lugha, wengine kudondoka na vifungo vilikatika kabisa kwa Jina la Yesu.


ROHO WA BWANA ALIKUWA JUU YA MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA NA MUNGU ALIMTUMIA KATIKA UPONYAJI KWA KIWANGO CHA JUU SANA 

KARIBU USHUHUDIE MATUKIO HAPA CHINI YA JINSI WATU WALIVYOKUWA WANAFUNGULIWA KUTOKA KATIKA VIFUNGO MBALI MBALI

Mama huyu hapa juu alikuja kwenye mkutano jijini Nagoya akiwa hawezi kutembea, wakati wa maombezi nguvu za Mungu zilishuka juu yake kwa namna ya kipekee na akaweza kutembea tena
UTUKUFU KWA YESU



Kiti cha matairi alichokuwa anakitumia mama huyu
Akimsifu Mungu Baada ya kuweza kutembea na kuachana na kiti baada ya kuombewa na Mchungaji Josephat Gwajima

Watu wa Mungu waliokuwa na matatizo mbali mbali na wakisumbuliwa na mapepo, pichani wako katika kuendelea kupokea uponyaji wao.







Mchungaji Josephat Gwajima akiwaombea mamia ya watu Baraka za Mungu..

Enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu, Mkiwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi. Ufufuo na Uzima tumekuwa tukiendelea na semina za kuwafundisha wachungaji wa mjini Nagoya Japan na mikutano ya watu wote iliyokuwa na mafanikio makubwa. Utukufu wa Mungu ulidhihirika kwa namna isiyokuwa ya kawaida.           






Comments