Kutana na Mtu wa Mungu Nabii Samson pale katika hema ya Kinabii
Geita kwaajili ya kufunguliwa kukombolewa kuwekwa huru kurejeshwa, kwa msaada
zaidi piga simu ni Bure 0756 809 209 Mtu wa Mungu,
Utangulizi:
Mambo yanayofanyika siku za
leo kote ulimwenguni ni Dalili halisi za kuonyesha kuwa kanisa la kristo
alilokusudia liwepo Duniani limehama katika nafasi yake, na Muovu ametumia nafasi hiyo kufanya kila jambo
analolitaka kutimiza kusudi lake na yeye,
Kanisa ni nini:
Tafsiri ya kanisa imetafsiriwa
na watu mbali mbali kwa mitazamo tofauti na mafunuo tofauti lakini katika hayo
yote majibu halisi yanatoka kwa mwenye kanisa ambaye ni Yesu Kristo ndiye
anayeweza kutuambia kanisa ni nini, tuangalie maneno yake mwenyewe juu ya kulijenga kanisa lake,
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu
nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu
haitalishinda. Mathayo 16:18,matendo 13:1,14:27,15:4 18:22
Sasa tumejifunza kwamba kanisa ni mtu aliyetayari kutumika na Mungu aliye
imara si kigeu geu, leo yupo kwa Mungu
kesho Kwa wachawi kesho , wewe ni wadhamani sana, hebu tuangalie mfano
mwingine juu ya kanisa
Sauli akaliharibu kanisa,
akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa Gerezani. Matendo ya mitume 8:3
Maandiko yote mawili yanadhibitisha kuwa Kanisa ni wewe na siyo jengo ila jengo linapata heshima baada ya wewe kukusanyikia humo sasa umenielewa kwamba nikisema rudi katika nafasi yako Ninamaanisha turudishe kanisa mahapi ambapo kiristo aliliweka, kumbuka niwapi Yesu amekuweka, ili urudi hapo haraka kabla gadhabu ya Mungu haijawaka juu yako,
Maandiko yote mawili yanadhibitisha kuwa Kanisa ni wewe na siyo jengo ila jengo linapata heshima baada ya wewe kukusanyikia humo sasa umenielewa kwamba nikisema rudi katika nafasi yako Ninamaanisha turudishe kanisa mahapi ambapo kiristo aliliweka, kumbuka niwapi Yesu amekuweka, ili urudi hapo haraka kabla gadhabu ya Mungu haijawaka juu yako,
Nini Ufanye ili kurudi katika nafasi yako,
Agizo langu ninawakumbusha
agizo nililopewa na Mungu juu yako,
Kwa sababu hii nimemtuma Timotheo kwenu, aliye mwanangu
mpendwa, mwaminifu katika Bwana, atakayewakumbusha njia zangu zilizo katika
Kristo, kama vile nifundishavyo kila mahali katika kila kanisa.1wakorintho
4:17
Namna pekee ya kurudi katika nafasi zetu ni toba ya kweli juu ya njia tulizozichagua sisi wenyewe tukaiacha njia ya uzima
tukaifuata njia ya mauti, kanisani unakuja lakini dhambi hutaki kuacha,
umechaguwa mauti ya umilele Dhambi ni
njia ya mauti, uwongo,uchawi,kuabudu sanamu,kuzini,kuzusha,uwoga,mizaha,
Na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. LUKA 24:47
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo
Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
Matendo ya mitume 20:28
Tumelipiwa gharama kubwa sana ambayo hakuna Mtu aliye na uwezo wa kuilipa hivyo tusichezee uwokovo tulionao ni ghali mno,
Tumelipiwa gharama kubwa sana ambayo hakuna Mtu aliye na uwezo wa kuilipa hivyo tusichezee uwokovo tulionao ni ghali mno,
Piga magoti anza kutubu, na
kukiri makosa juu ya toba
( marko 8:18 )wana macho lakini hawaoni wana
masikio lakini hawasikii,wana akili lakini hawakumbuki lolote, tumepitishwa katika mateso mengi bila ya kujuwa
wala kuona maana tulitekwa sasa basi,
leo mwisho warumi 8:1-6 Nahumu 1:9 Unawaza nini juu ya bwana ili akomeshe mateso
yako ili yasirudi kwa mara ya pili,
Maana nayajua mawazo
ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa
ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
Nami nitaonekana kwenu,
asema Bwana, nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya
ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza,
asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya
mchukuliwe mateka. Yeremia 29:11-14
Dhambi zinapofusha macho
zinaleta ukiziwi akili zinakamatwa haziwezi kukumbuka lolote, Mungu atusaidie
sana,
kusimama katika nafasi,
Mimi nitasimama
katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione
atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu.
Habakuki 2;1
Habakuki 2;1
Ndipo akalia kama simba, Ee
Bwana, mimi nasimama daima juu ya mnara wakati wa mchana, na kila usiku ninakaa
katika zamu ya ulinzi wangu.
Isaya 21 : 8
Isaya 21 : 8
Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.
Mathayo 14 : 25
Ukiwa katika nafasi yako yesu
atakukuta hapo hapo usikimbie tatizo lililo mbele yako Yesu anakuja siyo kivuli
chake,
Comments