YALIYOJIRI KATIKA KONGAMANO LA VIJANA CCC UPANGA JANA.


Picha: MOJA YA TULIYOJIFUNZA NI UTANDAWAZI NA MAADILI MEMA KWA VIJANA
Mchungaji   Mitimingi akifundisha  jana.
Jana jumatatu tarehe 07 April 2014 kulikuwa na kongamano kubwa la vijana lililofanyika katika ukumbi wa kanisa la City Christian Center(CCC Upanga). Mwalimu katika kongamano hilo alikuwa ni Mchungaji Peter Mitimingi. 

Maelfu wa vijana walihudhuria na hakika BWANA YESU alitwaa utukufu maana hata waliompokea kuwa BWANA na MWOKOZI wa maisha yao walikuwa ni wengi. 

Mchungaji  Peter Mitimingi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Huduma ya The Voice of Hope Ministry(VHM) alifundisha na katika Topic zilizogusiwa ni pamoja na

• AINA 10 ZA ZINAA
• MADHARA YA VIJANA KUJICHUA
• MADHARA YA KUANGALIA PICHA ZA NGOZO
• SABABU 10 ZA VIJANA KUFANYA TENDO LA NDOA KABLA
• UTHAMANI NA FAIDA ZA UBIKIRA KWA VIJANA
• MADHARA YA KUFANYA TENDO LA NDOA KABLA YA NDOA
• NJIA ZA KUDHIBITI TAMAA ZA MWILI
• ATHARI ZA MIGUSANO YA MWILI WAVULANA NA WASICHANA
• MTAZAMO WA MUNGU JUU YA MAISHA YA KIJANA


Haya ni baadhi ya matukio katika picha.MUNGU akubariki.
Baba Askofu Dr. Ranwel Mwanisongole Ndiye Aliyekuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano la Vijana
Waandishi wa Habari Pia Hawakuwa nyuma kuchukua habari kulikoni vijana kumiminika hapa leo!
Baadhi ya Vijana wakiwa kwenye Ukumbi wa Nje Baada ya Ukumbi wa Ndni kufurika Vijana walikaa nje na kufuatilia somo wakiwa nje
 Vijana wakifuatilia fundisho kupitia screen iliyowekwa kwa nje baada ya ukumbi wa ndani kujaa
BAADHI YA VIJANA WALIOPITA MBELE KUSALIMISHA MAISHA YAO KWA BWANA YESU KATIKA KONGAMANO LA VIJANA UPANGA CCC
MAKOMANDOO WA VHM HAWAKUWA MBALI KATIKA KUWAHUDUMIA VIJANA KWENYE KONGAMANO
VIJANA WALIOMPOKEA BWANA YESU WAKIJAZA FOMU MAALUM BAADA YA KUOMBEWA SALA YA TOBA KATIKA KONGAMANO LA VIJANA UPANGA CCC
VIJANA WALIFURIKA UKUMBI WA KANISA LA CCC UPANGA WAKIWA NA KIU NA SHAUKU YA KUPOKEA MAFUNDISHO




Comments