BWANA YESU
asifiwe ndugu yangu mpendwa.
Karibu tujifunze
ujumbe huu ambao MUNGU amenipa kwa ajili yangu na kwa ajili yako pia.
Dirii ni
kifaa cha cha kujikinga ili kuzuia
risasi au mishale ya adui kukudhuru.
Dirii
huvaliwa kifuani pote ambapo ni rahisi zaidi kumuua mtu, Moyo pia hukaa kifuani
na MUNGU anatuambia tulinde moyo kuliko yote tuyalindayo. Hapo umeona umuhimu
wa moyo na umeona umuhimu wa dirii.
Dirii ni kuzuia
silaha za adui.
Dirii ya
haki ni silaha za MUNGU Waefeso 6:11(Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
)
Ndugu yangu
usivae dirii tu ya kawaida bali vaa dirii ya haki.
Silaha za
MUNGU wakati mwingine inaitwa dirii ili kuweza kuzuia silaha zote za shetani
zisitudhuru.
Tunayo
mashambulizi mengi ya yule shetani lakini kwa kuwa kwetu na silaha za MUNGU au
dirii ya haki, shetani hatafanikiwa.
Waefeso 6:14( Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
)
-Watu
wamepoteza dirii zao na sasa wanatumia akili zao, ujanja wao na mbinu za
kipepo.
-Anania na
Safira walishindwa kutumia dirii kutumia dirii ya haki ila wakatumia ujanja wao
wenyewe, lakini wakakosa sana na kuharibikiwa.
KUNA MAWAZO YA HAKI YA AINA 2 KATIKA AGANO JIPYA.
1. KUSIMAMA KWA UADIRIFU.
-Kusimama kwa uadirifu ni kuhesabiwa haki
mbele za MUNGU Yakobo 2:23( Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu).
-MUNGU anatutazama sisi wanadamu ndani ya YESU KRISTO, zaidi ya
hapo hawezi kukuona kwa habari ya kukupatia haki, haki ya uzima wa milele au
haki yaw ewe ili adui asikudhuru maana anapomtazama YESU basin a wewe anakuona
uko ndani ya YESU.
-MUNGU anatuona sisi ndani ya Mwana wake
maana Mwana alitwaa dhambi zetu zote pale tulipomkiri yeye kuwa BWANA na
MWOKOZI wa maisha yetu.
· 2. TABIA NJEMA.
Tumerithishwa
tabia njema na MUNGU.
-MUNGU ameweka asili ya haki yake ndani yetu
kwa uwezo wa ROHO wake MTAKATIFU, hivyo MUNGU anatutaka kuishi kwa haki.
ILI KUISHI KWA
HAKI LAZIMA TUYAFANYE YAFUATAYO.
· 1. Kuwa na ni ya haki.
· 2. Kufikiri mawazo ya haki.
· 3. Kunena maneno ya haki.
MUNGU ANATAA.
1. Nia safi
2. Mawazo sahihi.
3. Utiifu kwake,
4. Kusema ukweli.
5. Kuwa waaminifu.
6. Kufanya kazi yetu kana kwamba YESU ndiye mkuu wetu.
7. Kuwatumikia wengine kwa furaha na haki.
ROHO MTAKATIFU ni ufunguo wa hayo yote hapo
juu.
-Ukimhudhunisha ROHO MTAKATIFU utakosa ulinzi.
-Ukikosa ROHO MTAKATIFU umeondoa ulinzi
maishani mwako.
-Neno la MUNGU likae kwa wingi mioyoni mwetu.
ROHO MTAKATIFU ni MTAKATIFU, Ndugu taka
utakatifu kwa kukubali kuwa na ROHO MTAKATIFU.
Ili tupokee utakatifu lazima tumpokee ROHO
MTAKATIFU.
Waefeso 4:30(Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi),
Ufunuo 3:4-6( Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao
uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa
wamestahili.
Yeye ashindaye atavikwa hivyo
mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima,
nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake.
Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
),
Waefeso 6:18 ( kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
)
Kwa leo naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
Comments