BWANA YESU
asifiwe ndugu yangu.
Nakukaribisha
tujifunze jinsi ya kudai haki zetu mbele za MUNGU.
Tunajua
tunadai haki kwa nani?
Haki zetu
tunazidai pale ambapo tunauhitaji wa jambo Fulani mbele za MUNGU.
Ni lazima
tumjue vyema tunayemdai.
Je tunasifa
za kudai hicho tunachotaka?
Isaya 54:17
(Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi
utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio
urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema
BWANA.
)
Watu wengi
hatujui jinsi ya kudai haki zetu mbele za MUNGU, Watu wengi hatufahamu tudai
nini, Watu wengi hua tunajaribu tu kudai lakini hatuna imani ya kupokea na
wengine hatujampokea BWANA YESU ambaye ndio chanzo cha haki yetu yote hivyo
hatuwezi kupokea.
Kuna haki
zinafahamika zinafahamika na kuna haki hatuzijui.
Muda mwingi
unawaza ‘’hivi MUNGU hanioni?’’
Wakati mwingine
unawaza ‘’Mbona Fulani kafanikiwa?’’
Yeremia 1:19
( Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema BWANA, ili nikuokoe. )
Tatizo sio
kujua ila tatizo ni kutambua haki yako mbele za MUNGU.
Tujikubali
kwa maneno na kwa matendo pia.
Haki ya
MUNGU haionekani kwa macho hadi pale haki yako itakapofanya kazi ndio utaona matokeo
mazuri.
Kutoka
15:1-18(Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia BWANA wimbo huu wakanena, na
kusema, Nitamwimbia BWANA, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda
farasi amewatupa baharini.
BWANA ni nguvu zangu, na wimbo
wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni MUNGU wangu, nami nitamsifu;
Ni MUNGU wa baba yangu, nami nitamtukuza.
BWANA ni mtu wa vita, BWANA ndilo jina lake.
Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.
Vilindi vimewafunikiza, Walizama vilindini kama jiwe.
BWANA, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, BWANA, mkono wako wa kuume wawaseta-seta adui.
Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.
Kwa upepo wa mianzi ya pua yako
maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu,
Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.
Adui akasema, Nitafuatia,
nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitaufuta
upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.
Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu.
Ee BWANA, katika miungu ni
nani aliye kama wewe? Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu,
Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?
Ulinyosha mkono wako wa kuume, Nchi ikawameza.
Wewe kwa rehema zako umewaongoza watu uliowakomboa, Kwa uweza wako uliwaelekeza hata makao yako matakatifu.
Kabila za watu wamesikia, wanatetemeka, Wakaao Ufilisti utungu umewashika.
Ndipo majumbe wa Edomu wakashangaa, Watu wa Moabu wenye nguvu tetemeko limewapata, Watu wote wakaao Kanaani wameyeyuka.
Hofu na woga umewaangukia;
Kwa uweza wa mkono wako wanakaa kimya kama jiwe; Hata watakapovuka watu
wako, Ee BWANA, Hata watakapovuka watu wako uliowanunua.
Utawaingiza, na kuwapanda
katika mlima wa urithi wako, Mahali pale ulipojifanyia, Ee BWANA, ili
upakae, Pale patakatifu ulipopaweka imara, BWANA, kwa mikono yako.
BWANA atatawala milele na milele.
).
-Maandiko
hapo juu yanaonyesha Musa na wana wa Israeli walitambua haki yako mbele za
MUNGU .
-Hapo juu
inaonyesha kwamba huwezi kumsifu mtu usiyemuona.
-Itambue
haki yak oleo kwa MUNGU.
-BWANA
amkekupa haki tena, unaweza kuomba
lolote kwake ukapata.
-Usijisahau
kwamba wewe ni mwenye haki, Palilia haki yako mbele za MUNGU siku zote.
BWANA YESU
asifiwe.
Usikubali
kulea tatizo ndani ya moyo wako.
Usilidharau
tatizo lako kwamba ni dogo sana bali shughulika nalo hata kama ni dogo sana.
Ndugu yangu
uliyekombolewa kwa damu ya YESU KRISTO, Baada ya kukombloewa ulitakaswa na
kupewa haki ya MUNGU katika KRISTO.
Lakini
wateule wengi wana UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIROHO.
-Haki yako
idai huku ukiwa na sababu kabisa kwamba haki yako ni halali kwako.
-Watu wengi
huona tu vinavyoonekana lakini visivyoonekana ni vibaya zaidi, visivyoonekana
ni mambo mabaya unayokusudia moyoni mwako.
Isaya
43:25-26 (Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.
Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.
).
Je unaijua
kesho yako katika MUNGU ikoje?
Mambo
mengine tunapanga sisi lakini tambua kwamba mengine MUNGU ndiye anapanga,
lakini MUNGU hakuwazii mabaya hata siku moja bali yeye anakuwazia mema tu.
Yeremia 29:11( Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya
amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
).
Palilia
maisha yako ya kiroho.
Palilia
safari yako ya mbinguni.
Mfuate ROHO
wa MUNGU siku zote za maisha yako.
Luka 18:1(Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba MUNGU sikuzote, wala wasikate tamaa.
)
Kwa leo naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
Comments