KUSHUGHULIKIA VIFUNGO


kushugulikia vifungo


Utangulizi:
Watu wengi wamefungwa  na hawajui kama wamefungwa  kwakuwa wengi wamezoea kuona kifungo cha kimwili  mtu kufungwa jele , Vifungo vipo vifungo vingi sana ambavyo vina watesa watu bila wao kufahamu
Kusala si kigezo cha Mtu kuwa Huru toka katika kifungo alichofungwa  unaweza ukawa unasali,unatoa mafungu ya kumi,unafunga mara kwa mara, inawezekana hatakuhudumu unahudumu lakini ukawa bado umefungwa,

Mara nyingi kupata urafiki au uhusiano  na mtu ni rahisi sana  lakini ili uweze kuendelea uhusiano wenu unatakiwa kuboresha mahusiano yenu, Maandiko matakatifu yanasema kuwa mtaijuwa kweli nayo hiyo kweli itawaweka Huru, ukishawekwa huru  fahamu kuwa kuna kazi ya zihada unatakiwa kuifanya,ili usifungwe tena,
KIZUWIZI NI NINI?

Kizuwizi ni hali au nguvu inayomzuwia Mtu katika kufanikisha jambo flani
Kwamfano,
Ø  Kutoolewa
Ø  Kuto owa
Ø  Kutofanikiwa kibiashara
Ø  Kutopata kazi
Ø  Kutopandishwa nafasi nyingine kazini (cheo)
Ø  Kutopendwa
Ø  Kuto sikilizwe,

Vizuwizi vipo vingi ila hapa kuna mfano mchache
AINA ZA VIFUNGO:
VIFUNGO VYA KIMWILI
VIFUNGO VYA KI-ROHO

Vifungo vya mwili tabia inaweza ikakufungia mambo yako mengi yasifanikiwe. Hivyo shetani anaweza kukuacha usonge mbele na kazi ya Mungu lakini akakuzuia kupitia vifungo vya tabia yako tabia ni kitu kidogo sana ila kinaweza kukuzuwia katika mambo makubwa sana, kwasababu kila mtu anapozaliwa anazaliwa na zawadi aliyopewa na Mungu yakumuwezesha yeye kuishi katika hii Dunia,
Chakwanza Kipawa,kipaji,nyota,Bahati, kipawa kimebatiswa majina mengi sana,
Chapili Tabia hii kwa sehemu motto anaweza akaridhi kidogo kwa wazazi sehemu nyingine kwake yeye mwenyewe, asipokuwa makini nyingine watu wanaridhi toka kwa marafiki au duniani kwa mazingira anayoyaishi,

KIPAWA NA TABIA YA MTU:
Kuna vitu kadhaa vya kuangalia Kama mtu wa Mungu unayehitaji kufanikiwa, cha kwanza ni kipawa na pili ni tabia yako mtu.

Mithali 18:16 “zawadi ya mtu humpatia nafasi, humleta mbele ya watu wakuu; ” hili neno zawadi kwenye Biblia ya kingereza linaitwa “GIFT” au kwa Kiswahili kipawa. Sasa basi kipawa cha mtu chaweza kumfikisha mbele za watu wakubwa na kujulikana. Mfano mtu anaweza kuwa na kipawa cha uwimbaji lakini anakaa kijijini na umaskini, ila kile kipawa chake kikionekana kinaweza kumleta mtu huyo mjini hii ndio maana ya sehemu ya kwanza ya andiko hilo. Kwasababu hiyo kila mtu aliyepo duniani amepewa kipawa na Mungu ambacho kwa hicho anaweza kufika kwenye hatua ya juu zaidi.
Mtu anaweza akawa hajasoma lakini kwa tabia yake Njema akapewa nafasi kubwa sana katika taasisi au kampuni, hayo tumeyeone makanisani tumeyaona,Makazini ni mifanomingine mingi unayo wewe, Tabia yako na kipawa chako kinauwezo wakukupatanisha hata na adui zako maana utapoinuliwa watalazimika kukujia

Tabia na kipawa kinavuta watu na kunakupaheshima bila ya kulazimisha, watu kukuheshimu,
Duwa na Maombi yangu kwako baada ya somo hili Maisha yako yabadilike kabisa Roho Mtakatifu akusaidie kukumbuka ulikopotezea kipawa chako na tabia yako,
 kipawa cha mtu humleta  kwenye mafanikio yake, tatizo linakuja pale mtu anapokuwa na kipawa lakini tabia yake si nzuri. Hivyo tabia ndio ambayo inakubakiza katika sehemu uliyopo. Mtu anaweza kuwa na macho ya rohoni au upako lakini kama tabia yake ni mbaya hakuna mtu atakayetamani kuwa karibu naye. Ili Mungu akutumie kwa kiwango cha juu ni muhimu kuanza kwa kubadili tabia yako  huitaji kuombewa wala kuwekewa mikono na watumishi wa Mungu wewe badilika tu,

TABIA ZA KIMUNGU NA TABIA ZA ASILI:
Biblia imeainisha tabia za aina mbili, yaani tabia ya Kimungu na tabia ya kiasili au ya mwilini. Katika 1Wakoritho 2:14 “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.” 1Wakorintho 3:1 kuna tabia za rohoni na tabia za mwilini. Hivyo anachosema Mtume Paulo ni kwamba unapoongea na watu inabidi ujue ama mtu huyo ana tabia za rohoni au za mwilini. Mfano mtu anaweza kuwa mwimbaji mzuri lakini ana tabia ya uongo; wewe ni shahidi mara Ngapi unawalika Mwiimbaji au mhubiri anawahaidi kuja kabisa mnatumia gharama nyingi kukusanya watu mwisho haonekani swali langu kwako je hiyo ni tabia Njema au Mbaya?
 Mtu mwingine anaweza kuwa na kipawa kitakachomfanya apate mchumba; lakini kama tabia yake ni mbaya ama uongo, au umbeya au uzinzi inaweza kumfanya kuachwa na Mchumba wake sio kwasababu hapendwi bali kwasababu ya tabia. Tabia ya Kimungu ni tabia njema na nzuri lakini tabia ya kibinadamu ni tabia mbaya aliyonayo mtu.

Shetani akitaka kuharibu kipawa cha mtu anaanzia kwenye tabia yake; kwa maana hiyo tabia ya kibanadamu au ya mwilini ndio hiyohiyo Biblia inaiita tabia ya kishetani. Ukisoma katika Yakobo 3:15 “Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani.” Unaona kumbe tabia mbaya ya kinadamu ndio hiyo inaitwa tabia ya kishetani. Mhubiri 10:1 “Mainzi mafu huvundisha marhamu ya mwuza marashi;  Kadhalika upumbavu haba ni mzito kuliko hekima na heshima.” Hili ni neno la hekima la Mfalme Suleimani kusema mainzi wanaweza kuharibu marhamu nzuri; ikimaanisha unaweza kupata mpenyo katika maisha lakini tabia mbaya inaweza kukupeleka mbali kabisa na upenyo wako.

Ndio maana waweza kumkuta mtu ni mwombaji au anatenda miujiza lakini tabia yake ikawa mbaya kwasababu ya asili. Jambo hili ndilo linalosabisha watu wengine kusema “kama ulokole ndio huu sitaki kuokoka” kumbe mtu huyo aliwahi kumuona mtu ambaye ameokoka na ananena au anaombea watu lakini ni mwongo au mzinzi. Katika Biblia, Samson alikuwa mnadhiri wa Mungu na alikuwa amepakwa mafuta tangu tumboni mwa mamaye.
Japokuwa alikuwa mpakwa mafuta lakini alikuwa na tabia mbaya ya kutaka wasichana wa kifilisti ambao Mungu alikataza tangu mwanzo. Hii ni sawa na mtu kung’ang’ania kufungwa nira na mtu asiyeamini.
Kwa njia hii Samson akakutana na Delila ambaye lengo lake halikuwa upendo bali ni kumharibia kipawa chake kwa kuijua siri yake. Vivyohivyo shetani amewaangamiza watu wa Mungu wengi kwa kuwafanya waoe au kuolewa na watu wasiomjua Kristo na matokeo yake kile kipawa cha Kimungu kilichokuwa ndani yao kinashindwa kuonekana tena.kimetitia kabisa unahitaji Msaada wa ushahuri na Maombi kwa Mtu wa Mungu  zamani punda akipotea watu walikimbia mbio kwa Mtu wa Mungu kuuliza siku za leo hawana Muda kabisa wa kuwauliza watu wa Mungu,


UFANYE NINI JUU YA HAYA? BADILISHA MWENENDO WA TABIA YAKO LEO:
Tabia mbaya ya mtu huondoka kwa kuamua mwenyewe, hata kama mchungaji akuombee mara zote kama tabia yako ni mbaya kwa asili inakulazimu kuamua kuibadili mwenyewe. Ni kweli tabia yako inaweza kuwa imeshakupotezea kibali kwa watu au imeshakupotezea upenyo katika maisha lakini ukiamua kuanza upya na BWANA na kuacha zile tabia mbaya Mungu wetu ni wa nafasi ya pili. Mungu wetu anatoa nafasi ya pili biblia inasema, “usifarahi ee adui yangu niangukapo mimi nitasimama tena” mwenye haka ananafasi saba za kuinuka ijapokuwa ataanguka, simaanishi ukajiangushe ili uinuke mara saba hapana aliyesimama asijisifu bali angalie asije kuanguka,

Leo naongea na watu ambao walikuwa waombaji leo hawaombi tena, walimuhofu Mungu lakini leo hawana hofu, walikuwa watakatifu lakini leo ni waovu wakubwa Mungu anayo nafasi ya pili kwaajili yako. Amua kutubu na kuacha dhambi na tabia hiyo mbaya; Mungu atakuwezesha tena kama alivyomwezesha Samson kuwaangamiza wafilisti wote. Hivyo uamuzi wa kwanza ni kuamua mwenyewe kuacha tabia hiyo.
Nimeamua kumtolea mfano Samson maana hakuna asiyejuwa mwanzo wa Samson na mwisho wake,
Hii ndiyo nafasi yako ya dhahabu
Kwamsaada na ushahuri wa  Maombi na Maombezi wasliana na
Mtu wa Mungu Nabii Samson
0756 809 209

Comments