KWANINI HATUPOKEI AU TUNACHELEWA KUPOKEA YALE AMBAYO TUMEOMBA KWA MUNGU?.




BWANA YESU atukuzwe watu wa MUNGU.
Namshukuru MUNGU kwa uzima aliotupa, na ushindi ambao anatupa kila siku.
Ndio maana sisi siku zote ni washindi , na tunashinda na zaidi ya kushinda kwa YESU aliyetupenda.
Ujumbe wa leo unazungumzia MATOKEO YA MAOMBI YETU.
Matokeo ya maombi yetu yanaweza kuwa ndio au hapana , yaani kupokea kile tulichoomba kwa wakati au kuchelewa kupokea kwa wakati na wakati mwingine tukokupokea kabisa.

ZIFUATAZO NI SABABU 11 ZA KWANINI TUNACHELEWA KUPOKEA AU HATUPOKEI KABISA KUTOKA KWA MUNGU KWA YALE TULIYOOMBA KWAKE.

   1. KUOMBA VIBAYA;  Yakobo 4:3 ( Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu. ).

   2.  HATUNA BIDII YA MAOMBI;   Mithali 8:17( Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. ).

    3.  KUTOMPENDA BWANA YESU;  Mathayo 11:28( Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. ),  

Yohana 14:6 (YESU akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa BABA, ila kwa njia ya mimi. )

Matendo 4:12( Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. ),

Yohana 14:14(Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya. ).

BWANA YESU asifiwe, hapa tunajifunza kwamba maombi yetu yote lazima tuombe katika jina la YESU KRISTO, Tena tunajifunza kwamba hakuna wokovu wala hakuna kupokea uzima wa roho na afya zetu kutoka kwingine kokote ila ni kwa BWANA YESU. Sasa kama hatumpendi BWANA wala hatumhitaji hatuwezi kupokea chochote kutoka kwa MUNGU hata kama tumeomba sana.

   4.    DHAMBI;  Isaya 59:1-2(Tazama, mkono wa BWANA haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na MUNGU wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia. ).

5.  TAMAA;   Yakobo 5:5( Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. ).

    6.  SHETANI;   Daniel 10:11-13 ( kaniambia, Ee Danielii, mtu upendwaye sana, yafahamu maneno nikuambiayo, ukasimame kiwima-wima; maana kwako nimetumwa sasa. Na aliponiambia neno hili, nalisimama nikitetemeka. Ndipo akaniambia, Usiogope, Danielii; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za MUNGU wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako. Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi. )

Shetani huzuia maombi, hivyo tunatakiwa tuitumie mamlaka ya KRISTO iliyo ndani yetu kumwadabisha maana ni mwoga sana kama sisi tukiwa na KRISTO YESU, Hapo juu tunaona kwamba alimzuia malaika ili majibu ya maombi ya Danieli yasifike kwa wakati.

    7.  HATUOMBI; Yakobo 5:16( Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. ).

    8.  KUTOKUSAMEHE;  Mathayo 6: 14-15( Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na BABA yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala BABA yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu. ).

   9.  MASHAKA;  Yakobo 1:6-7( la na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.  Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa BWANA. ).

    10.   KUKOSA MAARIFA YA NENO LA MUNGU; Hosea 4:6a( Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa). 
Mithali 1:7( Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.)
 

     11.    HATUNA IMANI ;  Yakobo 5:15( Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na BWANA atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa. )

BWANA YESU asfiwe.
Naamini umejifunza kitu na pia naamini umejua kikwazo chako cha kutokupokea ni nini. Kama ni dhambi acha dhambi, kama ni kukosa maarifa ya neno anza leo kujifunza neno la MUNGU pamoja na wenzako kanisani pia jisomee wewe mwenyewe. Kama kikwazo chako huna YESU KRISTO basi okoka leo ili uwe na haki ya kuomba na kupokea kutoka kwa MUNGU. Na kama kikwazo chako ni moja ya vipengele hapo juu, tengeneza ndugu na utaanza kupokea kwa BWANA.

 Kwa leo naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                     MUNGU akubariki sana .
                      Ni mimi ndugu yako
                       Peter M Mabula
                 Maisha ya Ushindi Ministry.
                           0714252292


Comments