Utawapenda uinjilisti choir, hapa wanaenda kuimba baadhi ya nyimbo zao kutoka katika albamu yao iliyozinduliwa leo. |
Katika uzinduzi huo zaidi ya Milioni 3 zilipatikana ambapo mgeni rasmi Eng Benjamini Mwendapole alitoa Milioni 1 na nusu . Hizi ni baadhi ya picha katika tukio hilo ambalo Maisha ya ushindi tulikuwepo na kushuhudia. Pia kama unataka DVD yajo ya albamu hii ya AWEZA KUTENDA TENA wasiliana nao kwa namba 0713504950, au 0652766281 na 0715425427
Wakati wa kusifu na kuabudu |
Samaria choir walikuwepo kuwasapoti Uinjilisti Choir |
Jerusalemu choir wakiwa kazini |
Kutoka kushoto ni mgeni rasmi, Eng Benjamini Mwendapole, Katikati ni Mchungaji Elly Boto kutoka KPC Kawe na kulia ni Askofu Philemon Phiri ambaye pia ndio mwenyeji. |
K P C Choir kama kawaida walikuwepo, Hapa wakijiandaa kuimba wimbo uitwao NIMEKOMBOLEWA KWA DAMU YA YESU. |
Ni zamu ya K PC Choir kuimba |
Ni live kabisa, safi sana vijana wa K P C |
Haleluya choir kutoka Morogoro wakiwasha moto wa injili iliyo hai. |
Kutoka Maisha ya ushindi Scholar alikuwepo. |
Watu walikuwa ni wengi sana, Hapa kwaya ya uinjilisti wakiingia stejini kwenda kuonyesha kwamba wanazindua video ya nyimbo bomba sana. |
Baadhi ya waliofika katika uzinduzi wa kwaya ya uinjilisti. |
Huku wakishangiliwa sana , kwaya ya uinjilisti mikocheni wakiwajibika , hapa wakiimba wimbo wa mwisha katika albam yao . Wimbo unaitwa MAISHA |
Askofu Philemon Phiri akipanda madhabahuni ili kuomba kwa ajili ya kuanza rasmi kwa uzinduzi. |
Watoto wa Mchungaji Froliani Katunzi, Majestic Singers walikuwepo, Hapa waliimba wimbo bora uitwao MIFUPA MIKAVU. |
Mgeni rasmi Eng Benjamini Mwendapole akikata utepe, na kununua DVD ya kwaya ya uinjilisti kwa Tsh. Milioni moja na laki tano. |
Mgeni rasmi pamoja na wageni wengine waalikwa wakipiga picha ya pamoja na kwaya ya uinjilisti Mikocheni A. EAGT |
Comments