Hatimaye Mungu amesikia maombi ya watu
wake baada ya mwimbaji wa zamani wa kanisa la Hillsong mwanamama Darlene
Zschech kumaliza matibabu ya kansa ya titi aliyoanza mwezi disemba
mwaka jana na hapo jana kufanikiwa kupanda madhabahuni kwa mara kwanza
toka aanza matibabu ya ugonjwa huo unaomaliza wengi.
Mwanamama huyo alitangaza tendo hilo
kubwa alilotendewa na Mungu wiki hii kwakushukuru maombi ya watu
waliokuwa pamoja naye bega kwa bega na kwamba hapo jana ilikuwa siku
yake ya kwanza kurejea madhabahuni kumtukuza Mungu katika kanisa
wanaloongoza na mumewe Mark liitwalo Hope Unlimited, toka aanze
matibabu.
Ambapo baada ya kumaliza na matibabu
hayo kwasasa mwanamama huyo anatarajia kuanza kupiga mionzi ili kumaliza
kabisa chembechembe za ugonjwa huo katika mwili wake.
Darlene anatambulika kama kiongozi wa muziki wa kisasa zaidi makanisani linapokuja suala la kusifu na kuabudu toka awe chachu ya mabadiliko ya muziki makanisani kupitia kanisa lake la zamani la Hillsong ambalo bado linasonga mbele na kushika nafasi za juu kwenye makanisa yanayopendwa kwa kuwekeza vyema kwenye muziki wa kisasa wa kumuinua Mungu.
credits:gospel kitaa
![]() |
Darlene akiongoza sifa kanisani kwake. |
Darlene anatambulika kama kiongozi wa muziki wa kisasa zaidi makanisani linapokuja suala la kusifu na kuabudu toka awe chachu ya mabadiliko ya muziki makanisani kupitia kanisa lake la zamani la Hillsong ambalo bado linasonga mbele na kushika nafasi za juu kwenye makanisa yanayopendwa kwa kuwekeza vyema kwenye muziki wa kisasa wa kumuinua Mungu.
credits:gospel kitaa
Comments