NGUVU YA MUNGU IMEONEKANA KATIKA IBADA YA MAAJABU ZANZIBAR.

MUNGU awabariki sana kwaya hii ambayo ni mfano wa kuigwa katika katika Zanzibar.
Leo Maisha ya ushindi tulikuwepo katika ibada, katika  kanisa la Pentecostal Assemblies of GOD( P A G) Chukwani Zanzibar. 
Kanisa hilo liko chini ya Mchungaji Amos Lukanula. ROHO MTAKATIFU ametuhudumia watumishi wake kwa ujumbe usemao ''USITUMIE VIBAYA MIAKA BA BARAKA AMBAZO MUNGU ANAKUJALIA KUPATA '' ambao ulifasiriwa na Askofu Joseph Masanja ambaye yuko hapa Zanzibar kihuduma.

Zifuatazo ni baadhi ya picha katika matukio ya ibada ya jumapili hii.


Kwaya ya PAG Chukwani walifanya kweli sana katika uimbaji.



Kutoka Maisha ya ushindi ni mimi ndugu yako Peter Mabula, katikati ni Askofu Joseph Masanja kutoka Mwanza na kulia ni Mchungaji Lucas Mpenzile ambaye pia ni mkurugenzi wa vijana jimbo la Dar es salaam. Tukiwa katika ibada ya kanisa la Pentecostal Assemblies of GOD( P A G) Chukwani Zanzibar. MUNGU alionekana na hakika YESU anaokoa, ukiamini unaokoka.

Siku ya furaha ni leo, wakati wa kufurahi ni sana . Yote ni katika BWANA YESU mwenye uzima.

Kwa YESU ni raha tena ni furaha harafu ni uzima ule wa milele.

Nimwabudu nani mimi kama sio wewe JEHOVAH, Hakuna mwingine wa kumwabudu ila ni wewe JEHOVAH.. Mtumishi wa MUNGU Baraka Mhunda akimwimbia MUNGU wimbo wa kuabudu.

Wakati wa neno la MUNGU ambalo lilifundishwa na Askofu Joseph Masanja kutoka Mwanza.

Askofu Joseph Masanja akihubiri katika jumapili ya leo.

Mchungaji Lucas Mpenzile akitabiri ushindi kwa kanisa.



Watumishi wa MUNGU Zanzibar wakiwa katika maombi katika

Wakati wa maombezi.

Wakati wa kusalimiana, watu wa Zanzibar wakarimu sana. Hapa nikisalimiana na watumishi mbalimbali baada ya ibada.



Nimebarikiwa sana na ibada ya leo.

Comments