Na Senior Pastor.JOHN KILIMA, UFUFUO NA UZIMA TANGA. |
Matendo 28:1
"Tulipokwisha kuokoka,ndipo tulipojua ya kuwa kisiwa kile chaitwa
melita"
Naliposoma andiko
hili nikafahamu ya kuwa mungu huruhusu jambo fulani baya likupate ili apate kukuvusha kutoka
hatua moja kwenda nyingine.
Kila tunapoendelea
kujifunza neno la mungu ndivyo tunaendelea kusonga mbele.
Mashindano ya dini
yanaweza kutokea kama tukitazama katika kitabu cha matendo ya mitume
:25:19"bali walikuwa na maswali mengine mengine juu yake katika dini yao
wenyewe,na katika habari ya mtu mmoja anaitwa Yesu, aliyekwisha kufa,ambaye
paulo alikaza kusema yu hai". Kwa
hiyo unaweza kupata tatizo fulani,kwa
ukiri wako wa kuwa Yesu Kristo ni Bwana na mwokozi wa maisha yako na alikufa na
akafufuka yu hai leo hata milele.
Hivyo tunapokumbana
na mikasa hiyo inabidi kusonga mbele kwa imani ile ile.
Pia tukisoma kitabu
cha nabii Isaya:10:26 imeandikwa"Na Bwana wa majeshi ataamsha mijeledi juu
yake.Kama vile alivyopiga midiani karibu na jabali la Orebu na fimbo yake
itakuwa juu ya bahari,naye ataiinua kwa namna ya kimisri".
Kwa hiyo
unapoendelea kusonga mbele kwa nguvu na
kupambana kwa imani ile katika ulimwengu wa roho , mungu mwenywe ambaye ni
bwana wa majeshi atafanya vita nao kwa
namna ya ajabu! Tena bwana asema katika Isaya:10:27"Tena katika siku hiyo
mzingo wako utaondoka begani mwako,na nira yake shingoni mwako,nayo nira
itaharibiwa kwa sababu ya kutiwa mafuta".
Neno nira ni kama
vifungo vyaweza kuwa vya mbao au chuma ili kwamba ufungwapo usitoke na ubaki
katika milki yao lakini Bwana wa majeshi
asema haijarishi ni nira ya namna gani itaharibiwa kwa kutiwa mafuta.
Kwa maana imeandikwa
katika Waefeso:6:12"kwa maana kushindana kwetu sisi si juu yadamu na
nyama;bali juu falme na mamlaka,juu ya wakuu wa giza hili,juu ya majeshi ya
pepeo wabaya katika ulimwengu wa roho". Kwa hiyo haya ni majeshi yanayo
tufatilia na inabidi tufanye vita nayo,tupambane nayo,tushindane nayo kwa jina
la yesu na kwa kuwa imeandikwa nao wakamshinda kwa damu ya mwana kondoo.
Vilevile tunaposhinda katika vita hivi dhidi ya ibilisi na majeshi yake Bwana Yesu Kristo
yuko pamoaja nasi kwa kuwa Mungu ni Bwana vita kama ilivyoandikwa katika kitabu
cha Joshua:5:12"Ikawa hapo Joshuwa
alipokuwa karibu na mji wa Yeriko,akavua macho yake na kuangalia,na tazama mtu
mume kasimama kumkabili mbele yake ,naye
alikuwa na upanga wazi mikononi mwake,Joshua akamwendea na kumwabia Je!wewe u upande wetu au upande
waadui zetu?Akasema la! Lakini nimekuja sasa,nili amiri jeshi la Bwana.Yoshua
akapomoka kiusouso hata nchi,naye akasujudu,akamwambia Bwana wangu ananiambia
nini mtumishi wake?".
Katika Matendo:28:3,5"Paulo alipokuwa amekusanya mzingo wa kuni na kuweka
motoni,nyoka akatoka kwa ajili ya ule moto akamzongazonga mkononi. Lakini yeye
akamtukusia motoni asipate madhara wao wakadhani atavimba au kuanguka chini kwa
kufa ghafla na wakiisha kumwangalia halimpati dhara lolote wakageuka na kusema
yeye ni mungu".
Kwa hiyo kwa
ushuhuda wa maisha yako katika Kristo Yesu wengine wanapata kuacha
maisha ya
dhambi na kumgeukia Mungu.Na dhara halikumpata Paulo, hivyo hatupaswi
kuishi
katika vifungo vy a shetani,umaskini,mogonjwa ,kufa ghafla,kukosa
kazi,kurogwa
na hivyo ni muhimu sana kuwapiga walinzi wangome kama vile
kutokuamini,hofu,wasiwasi ni walinzi wa ngome hao kama ilivyoandikwa
katika Matendo ya Mitume :4:1"hata wlipokuwa wakisema na watu
wale,makuhani na
akida wa hekalu na masadukayo wakawatokea".hii ina maanisha ni walinzi
wa
ngome hao hawataki ukombozi hao.
Hivyo nini hasa cha
kufanya?.Ila katika hili tunayo amri
kama ilivyoandikwa katika matendo ya mitume:10:1,16,:6:7,:16:15 kwa hiyo
tutakalonena ndilo litakwa.
Ndugu tunapaswa
kumshinda shetani katika roho kwa jina
la Yesu.
Amen.
Comments