BWANA YESU
asifiwe.
Mwanzoni mwa
mwaka 2009 yaani miezi michache tu baada ya kuokoka, BWANA alisema nami usiku baada tu ya kutoka kanisani . kwamba
mtu hataishi kwa mikate tu(Chakula) bali kwa neno la MUNGU. Muda huo huo nilipanga
kufunga kwa siku 3 bila kula wa kunywa chochote , nilifunga ila masaa 8 ya
mwisho nilishindwa kumaliza na kufungua. Nilisema nitafunga tena baada ya wiki
1 na kweli nilifanikiwa kufunga siku 3 na huo ulikuwa ni mwanzo mzuri sana
kwangu maana ilisababisha kuona mambo
mengi sana katika ulimwengu wa Roho. BWANA alinionyesha hata nguvu zangu za
kiroho, alinionyesha silaha zangu na ukubwa wake na jinsi ambavyo zinauwezo wa
kuangamiza mipango yote ya adui, alinionyesha maadui zaidi ya 100 wakinisaka
lakini kwa msaada wake niliwashinda wote. Ukweli kufunga ni muhimu sana kwa
kila mtu.
Kufunga
ndani yake kuna maombi Hivyo kufunga na maombi huambatana.Mtu akifunga harafu
hakuomba wakati wa kufunga kwake , mtu huyo amefanya tu mgomo wa kula .
Mathayo
17:21’’Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga’’
Miezi miwili
iliyopita niliota ndoto ya ajabu sana . Niliona nikiwa na watu wengi
ninaowafahamu na kila mmoja wetu alikuwa amejifunika shuka lake na kusinzia,
wengine wanakoroma isipokuwa mimi tu ambaye nilikuwa nimejifunika shuka ila
naangalia kutokea ndani ya shuka na kuona nje, ilichukua muda kidogo nikaona
mtumishi mmoja wa MUNGU katika wale
wanaofanya vyema sana katika injili Tanzania, akawa anawaangalia watu wote
tuliokuwa tumelala katika uwanja huo. Lakini cha ajabu wengine aliwaangalia
mara moja tu lakini mimi aliniangalia muda wote huku nikidhani hanioni ila mimi
ndio ninayemuona maana tulikuwa kimya sana kiasi kwamba angekuwa mtu wa kawaida
angejua wote tumelala, kumbe mimi sijalala. Mtu Yule ghafla akaniambia kwamba
‘’amka uombe, na tena omba sana, ‘’ nikaamka na kumwomba samahani maana kumbe
hakuwa mwanadamu wa kawaida, nikasimama huku wenzangu wote wamelala, nikasema
nitaomba akapotea. Wiki hiyo hakika ROHO MTAKATIFU alitaka niombe maana kuna
matukio zaidi ya 4 ya hatari sana yalitokea, sikufunga ila niliomba, moja ya
matukio yaliyotokea wiki hiyo ni kwamba siku 2 baada ya ndoto hiyo nilikuwa
natoka Kawe naenda Gongolamboto kupitia Buruguni kwenye daladala, tulipofika
kisiwa yaani kituo kimoja baada ya TMJ Hospital gari letu lilisimama ili kubeba
abilia wengine waliokuwa kituoni hapo lakini jambo la ajabu lilitokea ambapo
gari yetu ilipokaribia tu kusimama, watu waliokuwa nje walianza kupiga kelele
na kusema ‘’mnakufaaaaaaaaaaa’’ tukaanza kuwashangaa na mmoja wao akasema gari
yenu inawaka moto chini kote, kitendo kile kilipelekea watu kugombania mlangoni
ili kuokoa maisha yao, na nilishangaa mzee mmoja kikongwe sana ambaye
nilimpisha siti aliruka na kuwa wa kwanza kutoka nje , nikabaki nacheka. Wakati
watu wakigombania mlangoni Rohoni mwangu niliambiwa kwamba nisihofu ni amani
kubwa ipo. Nilishuka kwenye gari nikiwa wa mwisho na hakika nikakumbuka kwamba
ndio maana BWANA aliniambia kuomba siku ile maana alijua kipi kiko mbele yangu.
Konda na
dereva wake walianza kulaumiana na kusema wamesahau kuweka maji kwenye gari kwa
muda mrefu sana tukaanza gari inaungua moto na tukatembea hadi moroco kupanda
gari zingine tukaondoka. Ilikua ni hatari sana lakini BWANA YESU alisikia
maombi yangu ya wiki ambayo niliyaomba baada ya ndoto ile.
Leo tunazungumzia
habari za kufunga.
Kufunga ni
jambo muhimu sana kwa wateule wa KRISTO.
BWANA YESU
anatuambia kwamba Mengine tunayoyahitaji ili yafanikiwe tunahitaji kufunga na
kuomba.
Ninachotaka
kukuambia leo ni kwamba JE NI WAKATI GANI TUFUNGE?
Kuna nyakati 3 za kufunga kwa watu wa
MUNGU.
1. TUNAFUNGA
WAKATI AMBAO ROHO MTAKATIFU ANATUTAKA NA KUTUONGOZA KUFUNGA.
Luka 4:1-2 (
Na YESU, hali amejaa ROHO MTAKATIFU, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na ROHO muda wa siku arobaini nyikani,
akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.
).
ROHO MTAKATIFU
anatujua kuliko vile ambavyo sisi tunajijua, anapokuambia kufunga ni upendo
wake mkuu sana na ajabu sana maana yeye anajua yote yaliyopo na yajayo yote.
Hivyo kwa sababu unaishi na MUNGU ndani yako kama Biblia inavyosema basi mtii
yeye maana ndiye kiongozi mwema.
2. TUNAFUNGA
WAKATI AMBAO TUNAITWA NA VIONGOZI WA KANISA KWA AJILI YA KUFUNGA.
Waebrania
13:17 (Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa
ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye
hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.
).
Tusome tena Ezra 8:21( Ndipo nikaamuru kufunga, hapo penye mto Ahava, ili tupate kujinyenyekeza
mbele za MUNGU, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi
wenyewe, na kwa ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote.
)
Ezra hapa kama
kiongozi wa kundi au kama mfano wa viongozi wetu wa kanisa anaagiza kufunga
baada ya kuona jambo Fulani halijakaa vizuri. Nivizuri sana ndugu zangu tuwe
watii kwa vingozi wetu wa kanisa katika mambo kama haya maana hadi Mchungaji au
Askofu au Mtume au Nabii anasema kwamba tufunge ina maana katika ulimwengu wa
Roho kuna jambo ameona. Na yawezekana baada ya maombi hayo kuna ushindi mkuu
sana kwako na kwa kanisa hivyo usiache kufunga,
3. TUNAFUNGA
BAADA YA KUAMUA KUFUNGA.
Hii hua ni
kuchagua tarehe na kutenga ili kufunga hivyo ni jambo jema sana kwa kila Mkristo.
Kufunga
kunakusaidia wewe mwenyewe mfungaji.
Kufunga
kunakuboresha sana kiroho chako.
Maombi ya
kufunga huwapiga waliotumwa na shetani hata kama hawataki wataondoka tu ila ni
kufunga na maombi maana ukifunga harafu kwa muda wote huo wa kufunga kwako
ukawa kukuomba basi tambua kwamba ulifanya tu mgomo wa kula na sio kufunga ili
kupokea jambo kutoka kwa MUNGU.
-Kufunga kunaonyesha hitaji letu kuu kwa MUNGU
-Kufunga kusifanywe ili kujionyesha.
Kwa leo naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
Comments